• Nairobi
  • Last Updated April 25th, 2024 6:47 AM
Waislamu watakiwa kutumia kondomu

Waislamu watakiwa kutumia kondomu

Mipira ya kujikinga dhidi ya magonjwa ya zinaa na Ukimwi almaarufu kondomu. Picha/ Maktaba

Na WINNIE ATIENO

WAISLAMU nchini wametakiwa kutumia kinga aina ya kondomu ili kukabiliana na maambukizi ya magonjwa ya zinaa, hata hivyo baadhi ya waumini hao wamepinga hatua hiyo.

Kwenye maadhimisho ya siku ya kondomu duniani Jumanne, katika eneo la Pwani, mamia ya vijana walipewa kondomu ili wajikinge dhidi ya maambukizi ya ukimwi hatua ambayo ilipingwa vikali na viongozi wa kidini mbalimbali.

Shirika la kimataifa la kukabiliana na Ukimwi maarufu kama Aids Healthcare Foundation (AHF), lilisambaza takriban kondomu 300,000 kuwafaa wakazi wa Mombasa na kuwapima watu 600 ili wajue hali zao.

Mwaka 2017, shirika hilo lilisambaza takriban kondomu 4, 800, 000 kando na kupima watu 526, 618 waliojua hali zao.

“Mombasa pekee shirika letu liliwapima watu 108, 026 na kusambaza kondomu 1, 377, 544. Kondomu inatumika kama kinga ya magonjwa ya zinaa,” akasema mkurugenzi wa  kuhamasisha umma katika shirika hilo Faith Ndungu.

Afisa mkuu wa uhamasisho na mauzo wa shirika hilo duniani Terri Ford alisema ufadhili wa kondomu unakumbwa na changamoto dhidi ya ufadhili.

 

You can share this post!

Maadhimisho ya Siku ya Valentino yanoga

Wakazi Kisii waandamana kukejeli matamshi ya Babu Owino...

adminleo