• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 9:35 PM
Huzuni tele viongozi wakipoteza wazazi wao

Huzuni tele viongozi wakipoteza wazazi wao

Na WAANDISHI WETU

HUZUNI ilitanda jana katika familia za viongozi mbalimbali waliofiwa na wazazi wao. Rais Uhuru Kenyatta aliongoza taifa kutuma risala za rambirambi na faraja kwa kwa familia ya Kiongozi wa ANC Musalia Mudavadi kufuatia kifo cha Mama Hannah Atsianzale Mudavadi.

Marehemu, aliyekuwa na umri wa miaka 92, ni mjane wa marehemu waziri wa zamani Moses Mudavadi na mama wa aliyekuwa.

Rais alisema Mama Hannah atakumbukwa hususan kutokana na upendo wake kwa elimu na jinsi alivyosaidia watoto wengi werevu kutoka familia zisizojiweza kupata elimu bora.

Rais aliihakikishia familia ya Mudavadi kwamba yupo pamoja nao wakati huu mgumu wa msiba.Akihutubia wanahabari katika hifadhi ya maiti ya Lee jijini Nairobi, Bw Mudavadi alisema mazishi yatafanyika wiki moja baada ya kufungua Mwaka Mpya.

Wakati huo huo, Mbunge wa Mosop, Bw Vincent Tuwei alifiwa na babaye, Zakayo Cheruiyot Chebochok.Kwingineko, Mzee Joseph Kibii Koske ambaye ni baba wa Mbunge Mwakilishi wa Kaunti ya Kericho, Bi Florence Bore pia aliaga dunia.

Kwenye ujumbe wa rambirambi, Naibu Rais William Ruto aliwataja wote kama Wakenya waliojitolea kutumikia nchi kwa moyo mmoja na akatakia familia zao faraja.

Mbunge Mwakilishi wa Kaunti ya Wajir, Bi Fatuma Gedi, naye alimpoteza babake, Gede Ali ambaye alisemekana kufariki ghafla jijini Nairobi.

You can share this post!

Chama cha ‘wilbaro’ chapata mwanga wa kusajiliwa

Jubilee pazuri kutwaa ugavana Nairobi