• Nairobi
  • Last Updated April 23rd, 2024 7:55 AM
Watoto mayatima wafadhiliwa kuejerea darasani

Watoto mayatima wafadhiliwa kuejerea darasani

Na LAWRENCE ONGARO

WATOTO mayatima wapatao 100 wa Gatundu Kaskazini, wamefadhiliwa kwa vyakula huku wakiahidiwa kulipiwa karo shuleni mwaka wa 2021.

Kikundi cha wanawake likiongozwa na Jane Wambui kiliahidi kuwasaidia watoto hao ambao wanatoka vijiji vinne katika eneo hilo.

Watoto hao wanatoka viijiji vya Gakoe, Kanjuki, Ndiko na Kamwangi.

Bi Wambui alisema kwa muda mrefu watoto hao wamekuwa katika hali ngumu ya maisha na kwa hivyo wao kama wanawake walionelea kuwajali.

” Sisi kama kikundi cha wanawake Tutafanya juhudi kuona ya kwamba tunawasaidia watoto hao ambao kwa muda mrefu wamekuwa katika dhiki bila usaidizi wowote,” alisema Bi Wambui.

Alisema wengi wao hawakuweza kuhudhuria masomo na kwa hivyo wakaachwa katika hali ya ufukara vijijini.

“Sisi kama kikundi cha wanawake waliostaafu kama walimu tutafanya juhudi kuona ya kwamba watoto hao wanarudi shuleni na kupata masomo kamili,” alisema Bi Wambui kwa niaba ya wenzake.

Alisema wengi wa watoto hao ni wale walioachwa na wazazi wao huku wakiingilia vitendo viovu vijijini.

” Watoto wengi walioachwa yatima wamekuwa wakiingilia tabia zisizo dawa kama kuvuta sigara, na kunywa pombe haramu,” alisema mmoja wa wafadhili hao.

Alisema hawangetaka kuona watoto hao wakiingilia maovu bali ni vyema wakirekebishwa na kupewa usaidizi.

Wakati huo pia watoto hao waliathirika sana hasa wakati wa mlipuko wa homa ya covi-19.

” Wengi wao walikuwa wakirandaranda mitaani jambo ambalo ilikuwa ni hatari kwa maisha yao. Kwa hivyo tunataka kuwaleta pamoja ili wawe watoto wema,” alisema Bi Wambui.

You can share this post!

Mwaka 2020 ulivyosambaratisha mipango ya Waititu

Mwenye kilabu cha Balle Balle taabani kwa kulangua...