• Nairobi
  • Last Updated April 20th, 2024 7:55 AM
ULIMBWENDE: Ndizi na urembo

ULIMBWENDE: Ndizi na urembo

Na MARGARET MAINA

[email protected]

MBALI na kuliwa, ndizi zina manufaa mengine, hasa katika urembo wa ngozi.

Ndizi zina virutubisho muhimu vinavyoboresha ngozi.

Ndizi pia zina aina tatu za sukari zinazojulikana kama ‘sucrose’, ‘fructose’ na ‘glucose’.

Hakikisha unanawa uso wako mara mbili kwa siku. Unapofanya hivyo, unaondoa uchafu.

Ndizi husaidia kuzuia chunusi.

Hakikisha unanawa uso kwa sabuni ambayo inaendana na ngozi yako. Ikiwa ngozi yako ni ya mafuta, hakikisha unatumia sabuni ambayo itakuacha ukiwa mkavu na kama ngozi yako ina ukavu, jioshe na sabuni itakayokufanya uwe na unyevu.

Kulainisha ngozi

Changanya asali na ndizi kipande kimoja cha ndizi iliyopondwa na upake kwenye uso na shingo.

Nawa uso kwa maji fufutende baada ya muda wa nusu saa. Fanya hivi angalau mara moja kwa wiki.

Kung’arisha uso

Ndizi huwa na Vitamini C ambayo husaidia kuiweka ngozi kuonekana iking’aa. Kwenye ndizi iliyopondwa, ongeza vijiko viwili vidogo vya juisi ya limau na upake kwa uso na shingo. Osha kwa maji fufutende baada ya dakika 20.

Ni vizuri kupaka mchanganyiko huu wakati unataka kuenda kulala.

Kuzuia mikunjo

Ponda parachichi na ndizi pamoja. Paka kwa uso na uoshe baada ya muda. Mchanganyiko huu hulainisha ngozi ya uso na kuwa laini lakini pia hupunguza ukubwa wa matundu ya ngozi ya uso wako.

Kusugulia uso (Scrubing)

Changanya ndizi na sukari kijiko kimoja, kisha paka usoni na usugue taratibu. Ndizi hulainisha ngozi kavu na sukari huondoa seli zilizokufa kwenye ngozi.

Saga ndizi moja na Oats vijiko vitatu kisha changanya na asali na maziwa. Paka usoni kwa dakika 15 kisha sugua. Baada ya dakika 15 osha.

You can share this post!

Serikali yafunga shule yenye madarasa hatari Mukuru

Nairobi: Mutura afanya mabadiliko kiasi katika serikali yake