• Nairobi
  • Last Updated April 18th, 2024 9:15 PM
Mapishi ya samaki aina ya salmon

Mapishi ya samaki aina ya salmon

Na MARGARET MAINA

[email protected]

WAKATI mwingine mtu anakuwa amechoka na hangependa kupoteza muda jikoni.

Hivyo basi, kuandaa mlo wa haraka linakuwa ni wazo nzuri.

Mlo huu ni rahisi kuuandaa na hata haikuchukui zaidi ya dakika ishirini chakula kinakuwa tayari mezani.

Muda wa kuandaa: Dakika 15

Muda wa mapishi: Dakika 20

Walaji: 2

Vinavyohitajika

  • salmon fillet 2
  • viazi 2
  • mboga ya lettuce kiasi
  • nyanya 2
  • limau 1
  • saumu
  • chumvi
  • mafuta ya mizeituni

Maelekezo

Marinate samaki kwa kuhakikisha unaweka chumvi na kitunguu saumu kilichopondwa na nusu ya limau. Weke samaki pembeni.

Washa ovena kisha tia viazi ulivyovikatakata. Vikisha karibia kuiva, anza kupika samaki. Tia mafuta kidogo sana kama kijiko kimoja cha chai hivi katika kikaangio ambacho chakula hakishiki chini. Mafuta yakishachemka kiasi weka samaki wako (upande wenye ngozi chini kwanza).

Pika samaki mpaka uone rangi ya kahawia kwa chini kisha geuze upande wa pili.

Huku samaki wako akiwa anaendelea kuiva, tayarisha saladi yako kwa kusafisha mboga ya lettuce na nyanya kisha changanya pamoja. Kisha tengeneza salad dressing pembeni , kamua limau kisha tia mafuta ya mizeituni na chumvi kiasi.

Baada ya hapo samaki na viazi vitakuwa vimeiva. Andaa mlo wako na utakuwa tayari kuliwa.

You can share this post!

Mamia ya wakazi wakosa nafasi za wana wao katika shule za...

KOTH BIRO: Mechi za robo-fainali kugaragazwa Jumamosi hadi...