Na MARGARET MAINA
Muda wa kuandaa: Dakika 15
Muda wa mapishi: Dakika 30
Walaji: 4
Vinavyohitajika
Maelekezo
Safisha dagaa kisha waoshe na uwakaushe na taulo ya jikoni na uwaweke pembeni. Kisha katakata vitunguu na pilipili mboga kisha weka pembeni.
Baada ya hapo weka sufuria mekoni na umimine mafuta ya kupikia kwenye sufuria. Yakishapata moto, tia dagaa na uwakaange mpaka wawe wa kahawia.
Sasa tia kitunguu saumu, curry powder na tangawizi. Kaanga kidogo kisha malizia kwa kutia vitunguu maji, pilipili mboga, pilipili kichaa, chumvi na ukamulie juisi ya limau.
Kaanga kwa muda wa dakika tano na hakikisha vitunguu na pilipili mboga kwa pamoja haviivi sana na hapo dagaa watakuwa tayari.
Kusonga ugali
Kwanza unatakiwa kuchemsha maji ya moto, kisha koroga pembeni unga kiasi katika maji ya baridi na utie kwenye maji yanayochemka.
Fanya kama unatengeneza uji, uji wa ugali ukishachemka, tia unga na uanze kuusonga mpaka ugali uive. Ukishaiva pakua na dagaa tayari kwa ajili ya kuliwa.