• Nairobi
  • Last Updated April 23rd, 2024 9:40 PM
LISHE: Ugali na dagaa

LISHE: Ugali na dagaa

Na MARGARET MAINA

[email protected]

Muda wa kuandaa: Dakika 15

Muda wa mapishi: Dakika 30

Walaji: 4

Vinavyohitajika

  • dagaa wabichi
  • unga wa ugali kilo 1
  • nyanya ya kopo
  • vitunguu maji 2
  • limau ½
  • pilipili
  • chumvi
  • mafuta ya kupikia
  • pilipili mboga
  • kitunguu saumu
  • tangawizi
  • binzari ya curry

 

Maelekezo

Safisha dagaa kisha waoshe na uwakaushe na taulo ya jikoni na uwaweke pembeni. Kisha katakata vitunguu na pilipili mboga kisha weka pembeni.

Baada ya hapo weka sufuria mekoni na umimine mafuta ya kupikia kwenye sufuria. Yakishapata moto, tia dagaa na uwakaange mpaka wawe wa kahawia.

Sasa tia kitunguu saumu, curry powder na tangawizi. Kaanga kidogo kisha malizia kwa kutia vitunguu maji, pilipili mboga, pilipili kichaa, chumvi na ukamulie juisi ya limau.

Kaanga kwa muda wa dakika tano na hakikisha vitunguu na pilipili mboga kwa pamoja haviivi sana na hapo dagaa watakuwa tayari.

Kusonga ugali

Kwanza unatakiwa kuchemsha maji ya moto, kisha koroga pembeni unga kiasi katika maji ya baridi na utie kwenye maji yanayochemka.

Fanya kama unatengeneza uji, uji wa ugali ukishachemka, tia unga na uanze kuusonga mpaka ugali uive. Ukishaiva pakua na dagaa tayari kwa ajili ya kuliwa.

You can share this post!

Wanasoka chipukizi wafaidika kwa Sh16milioni baada ya...

Magoha asisitiza ni sharti wanafunzi waliojifungua warejee...