• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 4:31 PM
Chadema washindwa kumshtaki Magufuli ICC

Chadema washindwa kumshtaki Magufuli ICC

Na THE CITIZEN

MAAFISA wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) wameshindwa kushtaki serikali ya Rais John Pombe Magufuli katika Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu wa Kibinadamu (ICC) baada ya kesi yao kukosa kuungwa mkono na Kiongozi wa Mashtaka Fatou Bensouda.

Aliyekuwa mwaniaji wa urais kupitia Chadema, Tundu Lissu wikendi alisema, mawakili wa chama hicho hawaruhusiwi kuwasilisha kesi yao katika mahakama hiyo ya kimataifa iliyoko jijini Hague, Uswizi, bila kupitia afisi ya Bensouda.

Lissu aliyekuwa akizungumza katika mjadala wa mtandaoni, alisema Mkataba wa Roma unaruhusu tu kiongozi wa mashtaka wa ICC kuwasilisha kesi katika mahakama hiyo.

Chadema kilikuwa kimekusanya ushahidi ambao kilidai ulionyesha jinsi serikali ilikiuka haki za kibinadamu na kuwadhulumu viongozi wa upinzani kabla na baada ya uchaguzi mkuu Oktoba 28, mwaka jana.

 

You can share this post!

Facebook yaadhibu wafuasi wa Museveni

Matiang’i kupewa fimbo ya kuongoza jamii ya Gusii kisiasa