• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 2:07 PM
Kero mitandaoni Balala akiteua Mwingereza kupigia debe utalii

Kero mitandaoni Balala akiteua Mwingereza kupigia debe utalii

NA WANGU KANURI

Wakenya kupitia mitandao ya kijamii ya Twitter na Facebook wameeleza masikitiko yao kuhusiana na uamuzi wa Wizara ya Utalii wa kumteua mwanamitindo wa Uingereza Naomi Campbell kama balozi wa kimataifa wa Magical Kenya.

Akitoa tangazo hilo Januari 12, 2021, Waziri wa Utalii na Wanyamapori Najib Balala alisema kuwa Campbell alipewa jukumu la kustawisha Kenya kama utalii bomba na kusafiri duniani.

Katika ripoti, wizara hiyo ilisema kuwa kuteuliwa kwake kulifikiwa baada ya mkutano kati ya msanii huyo na Bw Balala.

“Tunawakaribisha katika habari za kufurahisha ambapo Naomi Campbell atatetea utalii na atasafiri barani kama balozi wa Magical Kenya,” Balala akasema katika taarifa kwa vyombo vya habari. Campbell kwa upande wake, alishukuru serikali ya Kenya kwa kuboresha usafiri Pwani, akiongeza kuwa kituo cha ndege cha Malindi kimefikia kiwango cha kimataifa.

“Nimevutiwa sana na ufasaha wa kiwango wa cheo cha dunia na muungano wa utaalamu wa gofu ulio katika Vipingo Ridge, muungano pekee uliopewa sifa Afrika nzima. Ninawakaribisha wataalamu wa gofu duniani kote kutembelea eneo hilo na kujifurahisha,” akasema.

Modeli huyo alikuwa Kenya katika likizo yake huku akiishi katika nyumba ya mapumziko ya bilionea mmoja ambaye inasemekana ilikuwa ya mchumba wake, mfanyibiashara wa Kiitaliano na aliyekuwa mkuu wa timua ya Formula One, Flavio Briatore.

Campbell, aliyekuwa katika safari yake ya tatu nchini Kenya, hata hivyo alidinda kuzungumza na vyombo vya habari na amekuwa akificha habari kuhusu safari yake huko Pwani kaskazini.

Wakati wa safari yake ya mwisho nchini Kenya, aliwafanya wengi kutoa maoni yao alipopiga picha akiwa uchi katika pahali pageni Malindi. Alitembea tena Malindi mwaka wa 2014 wakati wa likizo ya Krismasi lakini ili kuwasaidia watu.

Haya ni baadhi ya maoni ya Wakenya kuhusu kuteuliwa kwake, huku wengi wakisema kuwa jukumu hilo lingepewa Mkenya.

“Huo wadhifa wamepea Naomi Campbell sababu Lupita ni mzaha kwao?” akauliza @AdanZamuh.

“Taarifa kuhusu Naomi Campbell kuteuliwa kama balozi wa Magical Kenya ni upuzi. Vipi katika ardhi hii ya Mwenyezi Mungu, walimchagua Naomi badala ya Lupita Nyong’o? Mbona si Trevor Noah? Kivipi? Ama sababu Waziri anampenda? MAAJABU!” akakamilisha @DavidoOsiany.

“Wueh, ningependekeza Mulamwah badala ya mgeni Naomi Campbell na huyo mwanamke anayecheka peke yake,” akasema @MoseMungai.

“Inasikitisha sana kuona kuwa tunalipa wageni kama Naomi Campbell kustawisha Magic Kenya ulimwenguni ilhali tuna watu wenye umaarufu nchini Kenya kama Lupita Nyong’o wa Hollywood lakini punde tu Mkenya amestawi huko nje wanatuepuka kama Corona,” akateta @beatambutei.

Wengine, hali kadhalika walifikiri alikuwa chaguo bora.

“Naomi Campbell anastahili wadhifa huo wacheni ukabila,” akasema @IAm_Danniek.

“Ninafikiri Naomi Campbell anastahili wadhifa huo kama balozi. Ukifahamu kuwa audience walikuwa watu kutoka bara. Pia anaelewa mandhari ya nchi na amejihusisha na Kenya mara kadhaa; kwa hivyo anastahili cheo hicho na atafanikiwa kwake,” akasema @walowe_mlolwa.

“Anastahili. Naomi Campbell amekuwa akija Malindi kwa likizo za Disemba, kila mwaka kwa miaka mingi,” akaandika @John Musembi.

You can share this post!

CECIL ODONGO: Ushawishi wa mabaraza ya wazee kwenye mizani

Mwanamume wa familia ya Rais Kenyatta auawa Gatundu