• Nairobi
  • Last Updated March 19th, 2024 1:13 PM
Mwanamume wa familia ya Rais Kenyatta auawa Gatundu

Mwanamume wa familia ya Rais Kenyatta auawa Gatundu

Na MARY WAMBUI

WAPELELEZI wanachunguza kisa cha mauaji tatanishi ya Joseph Njuguna Mbeca, jamaa wa marehemu Chifu Mkuu Muhoho Gacheca.

Bw Gacheca ni babake mamake Rais Uhuru Kenyatta, Mama Ngina Kenyatta. Marehemu aliuawa Jumapili usiku na wakora nyumbani kwake katika kijiji cha Gatwikira eneobunge la Gatundu Kusini, Kaunti ya Kiambu.

Mkewe Gatheca, Teresia Wanjiru Njuguna ambaye pia alikuwepo nyumbani alikamatwa kama mshukiwa na hapo jana alifikishwa katika Mahakama Kuu ya Kiambu.

Kulingana na ripoti ya polisi, siku ya tukio, marehemu alikuwa amehudhuria mkutano wa baraza la wazee na akarejea nyumbani akiandamana na wazee watatu mwendo wa saa kumi na mbili jioni.

BW Gatheca na wazee wenzake walishiriki mlo wa nyama kisha wakanywa pombe ya kitamaduni hadi mwendo wa saa tatu za usiku ambapo wazee hao waliondoka kwenda zao.

Kama kawaida yake aliwasindikiza wageni wake hadi langoni lakini alipokuwa akirejea nyumbani akakamatwa na wanaume watano waliomburuta hadi ndani ya nyumba.

“Walimfungia mkewe katika chumba kimoja na kuanza kucharaza marehemu huku wakimwelekeza katika chumba cha kulala. Walipekuwa nyumba hiyo kisHa wakatoweka,” ikasema ripoti ya polisi.

You can share this post!

Kero mitandaoni Balala akiteua Mwingereza kupigia debe...

Ruto asukumwa ajiuzulu kwa kumkaidi Uhuru