• Nairobi
  • Last Updated March 19th, 2024 7:55 AM
Polisi wengi wagura kazi, walia wanalipwa mshahara wa kitoto

Polisi wengi wagura kazi, walia wanalipwa mshahara wa kitoto

Na Steve Njuguna

POLISI wengi wa akiba (NPRs) Kaunti ya Laikipia, wameacha kazi hiyo wakilalamika kwamba wanalipwa mshahara wa chini na kupokonywa silaha.

Polisi hao wamelaumu serikali kwa kuacha wakazi kwenye hatari ya kushambuliwa na majangili wanaotoka kaunti jirani.Mnamo 2019, serikali iliwapokonya silaha polisi wa akiba 3000 eneo la Kaskazini mwa Bonde la Ufa katika juhudi za kuangamiza ujangili.

Waliagizwa kurudisha silaha hizo katika vituo vya polisi ilipobainika baadhi yao walikuwa wakizitumia kwa vitendo vya uhalifu.Baadhi yao wanasema kwamba waliachwa bila uwezo wa kuwalinda wakazi wa maeneo yao baada ya kupokonywa silaha.

“Hatuwezi kusaidia maafisa wa polisi wahalifu wakivamia watu wetu kwa sababu hatuna silaha.

Hauwezi kwenda katika vita kupigana na adui aliye na bunduki ukiwa mikono mitupu kama baadhi ya wenzetu ambao wameuawa wakijaribu kusaidia maafisa wa polisi wakati wa mashambulizi,” alisema Bw Simon Ellman.

Alitaja kisa ambapo polisi wa akiba, Bw Simon Kipkemoi, aliuawa kwa kupigwa risasi na wezi wa mifugo. Bw Joel Kirui ambaye pia ni polisi wa akiba alisema tangu walipopokonywa silaha, wenzao 10 wameuawa.

You can share this post!

Maajabu ya pacha kufariki siku moja

Jubilee yaachia NASA chaguzi ndogo