• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 11:42 PM
Ruto azidisha uasi dhidi ya bosi wake

Ruto azidisha uasi dhidi ya bosi wake

PIUS MAUNDU na CHARLES WASONGA

NAIBU Rais William Ruto ameendeleza uasi dhidi bosi wake, Rais Uhuru Kenyatta kwa kuidhinisha wagombeaji katika chaguzi ndogo zitakazofanyika katika maeneo mbalimbali mwezi Machi mwaka huu.

Jana, Dkt Ruto aliongoza uzinduzi wa mfanyabiashara Urbanus Mutunga Muthama kuwa mgombeaji wa useneta wa Machakos kwa tiketi ya chama cha United Democratic Alliance (UDA) katika uchaguzi mdogo utakaofanyika Machi 18.

Kando na Machakos, Dkt Ruto pia amewadhamini Mbw Evans Kakai na Alex Lanya ambao watapeperusha bendera ya UDA katika chaguzi ndogo za maeneo bunge ya Kabuchai na Matungu, mtawalia.

Chaguzi hizo ndogo zitafanyika Machi 4. Shughuli hiyo ambayo ilihudhuriwa na wandani wake kutoka Machakos, wakingozwa na mwenyekiti wa UDA Johnstone Muthama, ilifanyika katika makazi rasmi ya Dkt Ruto mtaani Karen, Nairobi.

Hii ni licha ya chama cha Jubilee kutangaza kwamba kitaunga mkono wagombeaji wa vyama washirika wake katika handisheki katika chaguzi ndogo za Machakos na maeneo bunge ya Matungu na Kabuchai.

Lakini jana, siku moja tu baada ya Jubilee kutoa tangazo hilo, Dkt Ruto alimwidhinisha Bw Muthama, maarufu kama Ngengele ambaye anatarajiwa kushindana na mgombeaji wa Wiper, Bi Agnes Kavindu Muthama, Waziri wa zamani Mutua Katuku wa Maendeleo Chap Chap miongoni mwa wengine.

Bi Kavindu, ambaye alikuwa mwanachama wa Jopo la Maridhiano (BBI) anapigiwa upatu na Rais Kenyatta, ikizingatiwa aliwania kiti cha Mbunge Mwakilishi wa Machakos katika uchaguzi mkuu wa 2017 kwa tiketi ya Jubilee.

Mbunge wa Mwala, Vincent Musyoka alisema Bw Muthama ndiye aliibuka bora miongoni mwa wagombeaji 10 waliosaka tiketi ya UDA kulingana na kura ya maoni iliyoendesha na chama hicho ambacho alama yake ni wilbaro.

Katika siku za majuzi, Dkt Ruto amejitokeza kimasomaso kukaidi Rais Kenyatta. Mwishoni mwa wiki alimrukia bosi wake kwa kupendekeza rais atakayechaguliwa 2022 hapaswi kutoka jamii za Agikuyu ama Kalenjin.

kwa misingi kuwa ndizo pekee zimekuwa uongozini tangu Kenya ilipopata uhuru mnamo 1963.

You can share this post!

Pasta kusubiri Yesu korokoroni

Uchaguzi wa Nairobi wasitishwa tena