• Nairobi
  • Last Updated April 16th, 2024 4:01 PM
Ulinzi mkali mmoja akinaswa akiwa na bastola, risasi 500 eneo Biden ataapishwa kuwa Rais

Ulinzi mkali mmoja akinaswa akiwa na bastola, risasi 500 eneo Biden ataapishwa kuwa Rais

Na AFP

MWANAMUME aliyejihami kwa bastola na risasi zaidi ya 500 alikamatwa jijini Washington katika kituo cha ukaguzi wa kiusalama karibu na eneo ambapo rais mteule Joe Biden ataapishwa Jumatano.

Wesley Allen Beeler, kutoka Virginia, aliwasili katika kituo hicho cha ukaguzi mnamo Ijumaa na kujaribu kutumia stakabadhi bandia kuingia eneo hilo lililofungwa na ambalo liko karibu na jumba la Capitol, Amerika, kulingana na nakala zilizowasilishwa katika Mahakama ya Juu, jijini Washington, DC.

Maafisa walipokuwa wakikagua orodha ya watu walioruhusiwa kuingia, mmoja wao aligundua vibandiko vilivyokuwa nyuma ya gari la Beeler vilivyoandikwa “Dhuru Maisha,” na picha ya bunduki pamoja na ujumbe mwingine uliosema, “Wakijia bunduki zako, wape risasi zako kwanza.”

Alipokuwa akihojiwa, Beeler aliwaeleza maafisa kwamba alikuwa na bastola aina ya Glock katika gari lake.Msako ulianzishwa na kufichua bastola, risasi zaidi ya 500, na vifaa vinginevyo vya bunduki, nakala ya korti ilisema.

Beeler alikamatwa na mashtaka kuwasilishwa dhidi yake ikiwemo: kumiliki bunduki ambayo haijasajiliwa pamoja na kumiliki silaha kinyume na sheria, ilisema ripoti ya polisi.

Kufuatia kukamatwa kwake, Beeler alisema lilikuwa “kosa ambalo halikuwa maksudi” na kwamba yeye ni afisa wa ulinzi kutoka shirika la kibinafsi ambaye alipotea njia akielekea kazini karibu na Capitol.

Washington imemakinika mno kabla ya kuapishwa kwa Biden wiki hii, baada ya umati wa wafuasi wa Rais Donald Trump kuvamia jumba la Capitol mnamo Januari 6.

Watu watano walifariki katika shambulizi hilo akiwemo afisa wa polisi.Maafisa wa usalama wameonya kwamba wafuasi sugu wanaomuunga mkono Trump na ambao kuna uwezekano wamebeba vilipuzi, ni tishio kwa Washington pamoja na miji mikuu eneo hilo wakati huu.Maelfu ya vikosi vya polisi vimetumwa Washington huku mitaa eneo hilo ikifungiwa nje kwa vizuizi vya saruji.

Jengo la Kibiashara la Kitaifa ambalo kwa kawaida huwa limefurika watu kila baada ya miaka minne kwa hafla ya kuapisha rais, limetangazwa kuwa marufuku kuingia kufuatia ombi la kikosi cha ujasusi kinachohakikisha usalama wa rais.

Wakati huo huo, msaidizi mkuu wa Joe Biden alisema Jumamosi kwamba rais mpya atatia sahihi takriban mamia ya amri za rais katika siku yake ya kwanza afisini.Polisi wakihofia machafuko kutoka kwa wafuasi wa Trump walianzisha oparesheni ya kiusalama kote nchini humo kabla ya hafla ya uapishaji.

You can share this post!

Kioja waumini wakivunja makufuli sita kanisani

Jubilee inanidhulumu, alia mwaniaji ubunge Kabuchai