• Nairobi
  • Last Updated April 23rd, 2024 2:10 PM
Waganda washerehekea kurejeshwa kwa intaneti

Waganda washerehekea kurejeshwa kwa intaneti

MASHIRIKA na CHARLES WASONGA 

RAIA wa Uganda wamesherehekea kurejeshwa kwa huduma za mawasiliano ya intaneti ambazo zilizimwa siku chake kuelekea uchaguzi mkuu wa Januari 14, 2021.

Hata hivyo, mitandao mbalimbali ya kijamii ilisalia kufungwa na ingefikia tu kupitia mtandao wa siri (VPN).

Rais Yoweri Museveni ambaye aliibuka mshindwa na hivyo kupata nafasi ya kuendelea kuongoza Uganda kwa muhula wa sita, aliishutumu mitandao hiyo kwa kupendelea upande wa upinzani na “kutumiwa vibaya kuendeleza ajenda za wageni.”

Hata hivyo, Robert Kyangulanyi, almaarufu Bobi Wine, ambaye alikuwa wa pili katika matokeo rasmi yaliyotangazwa na Tume ya Uchaguzi, alidai kuwa serikali ya Museveni ilizima mawasiliano na intaneti na mitandao ya kijamii ili ifanikishe nia yake ya kuiba kura.

Naye Katiba Mkuu wa chama cha National Unity Platform (NUP) kilichodhamini Bw Wine, Joel Ssenyonyi alimshutumu Museveni kwa kuzima huduma za intaneti ili kuwazuia kuwasilisha ushahidi kuhudu udanganyifu katika uchaguzi huo.

Hata hivyo, aliwaambia wanahabari kuwa chama hicho kinaendelea kukusanya fomu za matokeo ya uchaguzi wa urais, zilizo na ushahidi wa udanganyifu.

Tume ya uchaguzi ilimtangaza Museveni mshindi kwa kuzoa asilimia 58.64 ya kura zilizopigwa huku Wine ambaye alikuwa mpinzani wake wa karibu akipata asilimia 34 ya kura.

Ushindi huo sasa unaashiria kuwa Museveni mwenye umri wa miaka 76 ataongoza Uganda kwa miongo minne (miaka 40) ikizingatiwa kuwa aliingia mamlakani mnamo 1986.

Makundi ya kutetea haki za kibinadamu imeshutumu vikali serikali ya Museveni kwa kuzima mifumo ya mawasiliano.

Wakati huo huo, maafisa wa usalama wanaendelea kuzingira boma la Bobi Wine viungani mwa jiji la Kampala huku mwanasiasa huyo akilalamika kuwa familia yake inakeketwa na njaa kwa kukosa chakula.

You can share this post!

Wanasiasa wanaofadhili ghasia Kapedo kukamatwa

Hotuba ya Uhuru yazidisha nyufa katika ngome yake