• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 8:55 PM
Seneta Mwaura aitaka serikali ijenge madarasa zaidi shule za umma

Seneta Mwaura aitaka serikali ijenge madarasa zaidi shule za umma

Na SAMMY WAWERU

SENETA Maalum Isaac Mwaura ameihimiza serikali kutengeneza madarasa zaidi katika shule za msingi za umma ili kusaidia kuzuia maambukizi ya virusi vya corona miongoni mwa wanafunzi.

Bw Mwaura alitoa ombi hilo kutokana na hali aliyoshuhudia baada ya kuzuru Shule ya Msingi ya Mwiki, Githurai, iliyoko katika eneobunge la Ruiru, Kiambu.

Alisema shule zenye idadi ya juu ya wanafunzi ni vigumu watoto kuzingatia kigezo cha umbali wa zaidi ya mita moja kati yao.

“Utaeleza vipi shule yenye zaidi ya wanafunzi 3,500 kama hii ya Mwiki watoto wazingatie umbali kati yao?” Seneta Mwaura akahoji.

Shule ya Mwiki ndiyo yenye idadi ya juu zaidi nchini ya wanafunzi.

Akieleza kusikitishwa na taswira ya shule hiyo hasa kutokana na upungufu wa ardhi, Bw Mwaura alipendekeza serikali kujenga mara tatu au nne zaidi ya idadi ya madarasa yaliyoko kwa sasa katika shule za umma nchini.

Shule zilifunguliwa rasmi mnamo Januari 4, 2021, miezi tisa baada ya kufungwa kufuatia mkurupuko wa janga la Covid-19 nchini.

Kwa sababu ya upungufu wa madarasa, ili kutii mikakati na kanuni zilizowekwa kusaidia kuzuia msambao wa corona, baadhi ya shule zimekuwa zikiendesha shughuli za masomo chini ya miti.

You can share this post!

Benzema afunga mabao mawili na kupaisha Real Madrid hadi...

Msihofu, tuko tayari kujaza nafasi za wakongwe Jelimo na...