• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 11:42 PM
Fikayo Tomori atua AC Milan kwa mkopo akitokea Chelsea

Fikayo Tomori atua AC Milan kwa mkopo akitokea Chelsea

Na MASHIRIKA

BEKI Fikayo Tomori wa Chelsea amejiunga na kikosi cha AC Milan kinachoshiriki Ligi Kuu ya Italia (Serie A) kwa mkopo.

Difenda huyo mwenye umri wa miaka 23 aliwajibishwa na timu ya taifa ya Uingereza kwa mara ya kwanza mnamo Novemba 2019.

Kwa mujibu wa gazeti la La Gazzetta dello Sport, AC Milan watakuwa radhi kumpa Tomori mkataba wa kudumu mwishoni mwa muhula huu na kujitwalia kabisa huduma zake kwa kima cha Sh3.5 bilioni.

Tomori ambaye alikosekana kwenye mipango ya baadaye ya kocha Frank Lampard uwanjani Stamford Bridge, aliwajibishwa na Chelsea mara nne pekee msimu huu huku akichezeshwa mara moja pekee kwenye Ligi Kuu ya Uingereza (EPL).

Sogora huyo alitia saini mkataba wa miaka mitano na Chelsea mnamo Disemba 2019 baada ya kuridhisha katika mchuano uliompa jukwaa la kuvalia jezi za Uingereza dhidi ya Kosovo.

Kabla ya Chelsea kumsajili beki mzoefu Thiago Silva kutoka Paris Saint-Germain (PSG) mwanzoni mwa msimu huu, Tomori aliwajibishwa mara kwa mara na kocha Lampard aliyewahi pia kumtia makali kambini mwa Derby County.

You can share this post!

Felix na Suarez waibeba Atletico dhidi ya Valencia ligini

Juventus wapepeta Bologna na kuendeleza presha kwa vikosi...