• Nairobi
  • Last Updated April 23rd, 2024 9:40 PM
Juventus wapepeta Bologna na kuendeleza presha kwa vikosi viwili vya jiji la Milan kileleni mwa jedwali la Serie A

Juventus wapepeta Bologna na kuendeleza presha kwa vikosi viwili vya jiji la Milan kileleni mwa jedwali la Serie A

Na MASHIRIKA

ARTHUR Melo alifunga bao lake la kwanza katika Ligi Kuu ya Italia (Serie A) mnamo Jumapili na kusaidia waajiri wake Juventus kuwapepeta Bologna 2-0.

Ushindi huo wa Juventus wanaotiwa makali na mwanasoka wao wa zamani Andrea Pirlo, uliwawezesha kutia presha zaidi kwa vikosi viwili vya jiji la Milan – AC Milan na Inter Milan wanaoshikilia nafasi mbili za kwanza kileleni mwa jedwali.

Melo ambaye ni raia wa Brazil aliyesajiliwa kutoka Barcelona ya Uhispania mwanzoni mwa msimu huu, aliwaweka Juventus kifua mbele katika dakika ya 15 kabla ya Weston McKennie kufunga la pili katika dakika ya 71.

Licha ya kupigwa na Atalanta 3-0 mnamo Januari 23, AC Milan wangali wanaselelea kileleni mwa jedwali kwa alama 43, mbili zaidi kuliko Inter waliolazimishiwa sare tasa na Udinese katika mchuano mwingine.

AS Roma wanafunga mduara wa tatu-bora kwa alama 37, moja zaidi kuliko Juventus na Atalanta wanaoshikilia nafasi za nne na tano mtawalia.

Mechi dhidi ya Bologna ilikuwa ya 19 kwa Melo kuchezea Juventus waliojitwalia huduma zake kutoka Barcelona kwa kima cha Sh9 bilioni.

Goli lililopachikwa wavuni na McKennie ambaye ni raia wa Amerika, lilikuwa lake la nne kutokana na mechi 21 zilizopita akichezea Juventus waliomsajili kutoka Schalke 04 ya Ligi Kuu ya Ujerumani (Bundesliga) mwishoni mwa msimu wa 2019-20.

MATOKEO YA SERIE A (Januari 24):

Juventus 2-0 Bologna

Genoa 1-0 Cagliari

Verona 3-1 Napoli

Lazio 2-1 Sassuolo

You can share this post!

Fikayo Tomori atua AC Milan kwa mkopo akitokea Chelsea

ODONGO: Kura ya Matungu ni jukwaa kwa Mudavadi kuonyesha...