• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 12:58 PM
Ruto apangia UDA mikakati ya chaguzi ndogo

Ruto apangia UDA mikakati ya chaguzi ndogo

Na ERICK MATARA

NAIBU Rais William Ruto ameanza mikakati ya kuhakikisha chama chake kipya cha United Democratic Alliance (UDA) kimeshinda viti vya udiwani katika chaguzi ndogo zijazo.

Tayari Dkt Ruto amekutana na Seneta wa Nakuru, Bi Susan Kihika kuweka mikakati ya UDA kutwaa ushindi katika chaguzi ndogo za wadi za Hell’s Gate na London, Kaunti ya Nakuru.

Viti hivyo, vilisalia wazi kufuatia vifo vya diwani wa London, Samuel Mbugua na mwenzake wa Hell’s Gate, John Njenga mnano Novemba mwaka uliopita.

Chaguzi hizo ndogo zitafanyika Machi 4.

Huku wandani wa Dkt Ruto wakiwapigia kampeni kali wawaniaji wa UDA, Gavana Lee Kinyanjui na Mbunge wa Nakuru Magharibi,Samuel Arama wamekuwa wakivumisha wawaniaji wa Jubilee.

Jubilee imekuwa ikidhibiti siasa za Nakuru tangu 2013, lakini sasa huenda ikapoteza umaarufu kwa kuwa wabunge wengi wa eneo hilo pamoja na Bi Kihika wamehamia mrengo wa Dkt Ruto.

You can share this post!

Raila aambia Mlima Kenya wamlipe ‘madeni’ yake 2022

BI TAIFA JANUARI 26, 2021