• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 5:22 PM
Mkopo wa Ighalo kambini mwa Man-United watamatika rasmi

Mkopo wa Ighalo kambini mwa Man-United watamatika rasmi

Na MASHIRIKA

FOWADI raia wa Nigeria, Odion Ighalo amesema kwamba “ndoto yake ya kuendelea kuhudumu uwanjani Old Trafford imetamatika” kadri anavyozidi kujiandaa kuondoka kambini mwa Manchester United baada ya kipindi chake cha mkopo wa mwaka mmoja kukamilika.

Ighalo, 31, alifungia Man-United mabao matano kutokana na mechi 23 tangu asajiliwe na miamba hao wa soka ya Uingereza kutoka kikosi cha Shanghai Shenhua ya Ligi Kuu ya China (Chinese Super League).

“Nitashukuru siku zote usimamizi wa Man-United kwa fursa hii adimu waliyonipa. Nitasalia kuwa shabiki mkuu wa Man-United popote nitakapokuwa,” akaandika fowadi huyo kwenye ukurasa wa akaunti yake ya mtandao wa kijamii wa Twitter.

Kipindi cha kuhudumu kwa Ighalo uwanjani Old Trafford kinatarajiwa kutamatika rasmi mnamo Januari 30, 2021.

Tangu atue guu kambini mwa Man-United, Ighalo amewajibishwa katika jumla ya michuano tisa pekee ya Ligi Kuu ya Uingereza (EPL) na nafasi yake katika kikosi cha kwanza ilitwaliwa kabisa na nyota Edinson Cavani aliyesajiliwa kutoka Paris Saint-Germain (PSG) ya Ufaransa mnamo Oktoba 2020.

You can share this post!

NDIVYO SIVYO: Aisee ndugu zetu wanahabari, tetesi si kisawe...

Amina matumaini tele Kenya itapata idhini ya kuandaa Riadha...