• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 11:05 AM
Biden aondoa marufuku ya Trump kuhusu uavyaji mimba

Biden aondoa marufuku ya Trump kuhusu uavyaji mimba

Na AFP

WASHINGTON DC, Amerika

RAIS Joe Biden ameondoa marufuku yaliyozuia Amerika kutoa misaada ya kifedha kwa mashirika ya ng’ambo yanayotoa ushauri kuhusu uavyaji mimba.

Biden alisema hatua hiyo ni miongoni mwa ambazo serikali yake inachukua kuimarisha afya.

“Ni sera ya serikali yangu kusaidia afya na haki ya afya ya uzazi ya wanawake nchini Amerika na kote ulimwenguni,” Biden alisema kwenye amri ya kuondoa marufuku hiyo.

Alisema marufuku hiyo ilihujumu juhudi za Amerika za kutetea usawa wa jinsia ulimwenguni.

Biden pia aliagiza kubadilishwa kwa kanuni zilizoanzishwa na serikali ya mtangulizi wa wake Donald Trump zilizozuia serikali kufadhili kiliniki zinazowatuma wanawake kuavya mimba.

Saa chache baada ya amri ya Biden, waziri wa afya Antony Blinken alitangaza kuwa wizara yake itatoa msaada wa Sh3.25 bilioni kwa shirika la United Nations Population Fund.

Serikali ya Trump ilisitisha ufadhili kwa shirika hilo likidai lililazimisha watu kuhasiwa na kuavya mimba nchini China.

Blinken pia alisema Amerika itaondoa jina lake katika azimio la 2020 Geneva Consensus Declaration ambalo mataifa 30 yalipitisha kupinga uavyaji mimba.

You can share this post!

Uingereza yapiga marufuku wasafiri kutoka Burundi na Rwanda

Washukiwa saba, silaha 35 zanaswa katika operesheni...