• Nairobi
  • Last Updated April 20th, 2024 6:55 AM
Walimu waililia serikali iwalinde dhidi ya ugaidi

Walimu waililia serikali iwalinde dhidi ya ugaidi

Na Manase Otsialo

CHAMA cha Walimu nchini (KNUT) kimeitaka serikali ihakikishe usalama unaimarishwa Kaunti ya Mandera ili masomo yarejee kama maeneo mengine nchini.

Akihutubia walimu baada ya kuchaguliwa tena, Katibu Mkuu wa KNUT eneo hilo, Bw Mohammed Kulo, alisema serikali ina jukumu la kuhakikisha masomo yanarejea katika mji kaunti hiyo ya mpakani iliyoathiriwa na vita baina ya majeshi ya Somalia na Jubbaland.

“Serikali ya Kitaifa lazima ihakikishe usalama unaimarishwa Mandera ili walimu wafanye kazi yao bila kusumbuliwa. Kukataa kutekeleza wajibu hao na kisha kuhamisha walimu ni kuhujumu elimu ya watoto wetu,” akahoji Bw Kulo.

Afisa huyo alisema serikali imekuwa ikiibagua kaunti hiyo kwa kuwa kuwapa walimu uhamisho hadi maeneo mengine badala ya kumakinikia usalama wao kazini.

‘Serikali ina jibu kwa kila tatizo nchini. Kukataa kuwahakikishia walimu usalama wao hapa Mandera kisha kuwahamisha ni kuhujumu elimu ya watoto wetu,’ akasema Bw Kulo huku akitoa wito walimu wengi waajiriwe katika kaunti hiyo.

Mandera inakumbwa na uhaba wa walimu 1894 katika shule za msingi na 517 katika shule za upili.

 

 

You can share this post!

WANTO WARUI: TSC imejifunga kibwebwe kuporomosha KNUT...

TAHARIRI: Tusiwe na pupa ya kurudisha kiboko