• Nairobi
  • Last Updated April 20th, 2024 6:55 AM
Wanafunzi wafeli majaribio ya KCPE kwa wingi

Wanafunzi wafeli majaribio ya KCPE kwa wingi

Na DAVID MUCHUNGUH

WANAFUNZI wengi walianguka mtihani wa majaribio wa Darasa la Nne waliofanya mwaka jana na kuibua wasiwasi kuhusu iwapo wamejiandaa vyema kwa mtihani wa mwisho watakaofanya siku 48 kuanzia Jumatano.

Wanafunzi wa shule za umma walifanya vibaya zaidi katika mtihani huo wa majaribio kuliko wale wa shule za kibinafsi.

Baraza la Taifa la Mitihani (KNEC) linasema kuanguka huko katika shule za umma kulisababishwa na kufungwa kwa shule wakati baadhi ya wanafunzi wa shule za kibinafsi walikuwa wakisoma kupitia mtandao.

Mtihani huo ulifanywa na wanafunzi wa darasa la nane, gredi ya nne na kidato cha nne waliporejea shuleni Oktoba mwaka jana. Wanafunzi wa madarasa mengine walirudi shuleni Januari 4 mwaka huu.

“Moja ya matokeo ya utafiti wa Knec ni kwamba wanafunzi wengi wa darasa la nane walifeli. Hii inathibitishwa na idadi kubwa ya wanafunzi ambao hawakupata asilimia 50 katika masomo mengi,” inaeleza ripoti.

Wanafunzi walio maeneo kame na yale masikini walipata matokeo mabaya. Knec inahusisha hatua hii na ukosefu wa tekinolojia ya habari na mawasiliano kuwawezesha kusoma wakati shule zilikuwa zimefungwa kutokana na janga la corona.

“Ni wazi kuwa wanafunzi wengi wa darasa la nane hawajafikia viwango vinavyohitajika katika masomo husika,” inaeleza ripoti hiyo.

Mitihani hiyo ilifanywa na kusahihishwa na walimu ambao walituma alama ambazo wanafunzi walipata kwa Knec kuchanganua.

Wanafunzi wengi walifeli hisbati na somo la ishara, Kiingereza na Kiswahili.

You can share this post!

Joho na Kingi waongoza mipango ya kuhama ODM

Masaibu ya Sonko yazidi huku kesi zikifufuliwa