• Nairobi
  • Last Updated April 16th, 2024 4:55 PM
Festus Mwoki ashinda mbio za nyika za Pwani

Festus Mwoki ashinda mbio za nyika za Pwani

NA ABDULRAHMAN SHERIFF

FESTUS Mwoki alitumia muda wa dakika 30 nukta 05 na kuibuka mshindi wa Mbio za Nyika za Kaunti ya Mombasa za kilomita 10 zilizofanyika uwanja wa Mbaraki Sports Club.

Mwoki alifuatiwa na Muturi Nzemba aliyekimbia kwa muda wa dakika 30.30 hali Jared Kiptanui akawa watatu kwa kutumia dakika 30.45. Nafasi ya nne ilinyakuliwa na Hillary Kipngetich aliyemaliza kwa dakika 30.50.

Peter Kangethe alitumia muda wa dakika 30.55 na kuwa watano hali veteran Erick Shikuku na Ibrahim Hamisi wakawa wa sita na wa saba baada ya kutumia dakika 31.05 na 31.25 mtawalia. Mwanamke wa pekee aliyeshiriki alikuwa Gladys Mutisya alimelazima mbio hizo kwa dakika 35.30.

Kulingana na Katibu wa Chama chas Riadha cha Kenya (AK) tawi dogo la Mombasa, Beatrice Taita washiri waliomaliza nafasi za tano za kwanza ndio watawakilisha Mombasa kwenye Mbio za Nyika za jimbo la Pwani zitakazofanyika uwanja wa Dawnson Mwanyumba Jumamosi ijayo.

Beatrice alimshukuru Mwenyekiti wa Chamber of Commerce wa Mombasa, Mustafa Ramadhan kwa kudhamini mbio hizo. “Ramadhan amedhamini mbio hizo na hatuna budi kumshukuru kwa kujitolea kwake kusaidia mchezo huu,” akasema.

You can share this post!

Olunga apimwa corona kujiandaa kwa Kombe la Dunia la Klabu

Mamelodi Sundowns yatinga 16-bora Nedbank Cup bila Mkenya...