• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 11:42 PM
Dereva Chager kutumia mashindano ya Autocross Kasarani kujiandaa kwa mbio za magari za KCB Nakuru Rally

Dereva Chager kutumia mashindano ya Autocross Kasarani kujiandaa kwa mbio za magari za KCB Nakuru Rally

Na GEOFFREY ANENE

BINGWA wa mbio za magari nchini Baldev Chager ni miongoni mwa madereva 48 ambao wamethibitisha kushiriki duru ya pili ya mashindano Autocross yanayodhaminiwa na benki ya KCB.

Duru hiyo itafanyika katika uwanja wa mbio za magari wa Kasarani ambao baadaye 2021 utatumika kwa Mbio za Magari za Dunia za Safari Rally.

Chager, ambaye alikuwa juu ya jedwali la Mbio za Magari za Kitaifa za Kenya (KNRC) 2020 kabla ya mashindano kusimamishwa kutokana na masharti ya kuzuia kuenea kwa virusi vya corona, ameingia katika kitengo cha “Open Class” pamoja na Kirit Rajput anayeongoza msimu wa Autocross mwaka 2021, Asad Khan “Kalulu”, Hamza Anwar na mwanadada nyota wa mbio za pikipiki Maxime Wahome.

Anish Chouhan pia atawania ubingwa wa kitengo hicho ambacho kinatarajiwa kuwa kivutio cha Jumapili.

Chager anatumia mbio za Autocross kujiandaa kwa duru ya kwanza ya Mbio za Magari za kitaifa zitakazofanyika katika Kaunti ya Nakuru mnamo Februari 20.

You can share this post!

Gharama ya maisha kupanda kufuatia ongezeko la bei ya mafuta

Moise Kean afungia PSG tena na kuwaongoza kutua kileleni...