• Nairobi
  • Last Updated April 24th, 2024 10:40 AM
Mutua alia Kalonzo ameteka BBI Ukambani

Mutua alia Kalonzo ameteka BBI Ukambani

Na Pius Maundu

GAVANA wa Machakos Dkt Alfred Mutua amemlaumu kinara wa Wiper, Bw Kalonzo Musyoka, kwa kuteka mchakato wa kurekebisha Katiba kupitia BBI katika kaunti hiyo.

Alibashiri kwamba Wakenya watakataa BBI iwapo Rais Uhuru Kenyatta na kiongozi wa ODM, Bw Raila Odinga, wataruhusu viongozi wanaootea siasa za urithi kwenye uchaguzi mkuu wa 2022 kuteka mchakato huo.

“Ikiwa yanayotendeka Machakos ndivyo ilivyo kote Kenya, basi nabashiri BBI itasambaratika. Tunatoa onyo kwa Rais na Raila Odinga kwamba viongozi wanahujumiwa katika kampeni za BBI, na wasipokuwa waangalifu Wakenya watakataa BBI. Ikiwa kitu ni kizuri kinafaa kufanywa vyema” alisema Alhamisi ofisini mwake.

Alikuwa ameandamana na madiwani 34 wa Kaunti ya Machakos ambao walilaumu kamati ya BBI kwa kuwapuuza magavana wa kaunti za Ukambani na kumtumia Bw Musyoka kupigia debe mswada wa kubadilisha katiba.

You can share this post!

Shinikizo Ruto na Gideon Moi waungane

Mpango wa ‘Happy Hour’ warejeshwa kupunguza...