• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 8:55 PM
Kila familia kulipa Sh6,000 katika mageuzi mapya NHIF

Kila familia kulipa Sh6,000 katika mageuzi mapya NHIF

Na Otiato Guguyu

KILA familia italazimika kulipa ada ya lazima ya Sh500 kwa Mpango wa Bima ya Afya Nchini (NHIF) huku serikali ikiandaa bima ya afya kwa Wakenya wote.

Waziri wa Fedha Ukur Yatani alisema kila familia itatozwa Sh6,000 kila mwaka ili kujumuishwa katika Mpango wa Afya kwa Wote (UHC) kwa huduma za wagonjwa waliolazwa na wasiolazwa ikiwemo huduma za uzazi, matibabu ya maradhi ya figo, saratani na upasuaji.

“Lengo la serikali ni kubuniwa kwa mpango wa lazima wa UHC utakaosimamiwa na NHIF na kudhibitiwa na Wizara ya Afya na kutumika kama mpango wa kitaifa kwa raia wote wa Kenya pasipo kujali hadhi ya mtu katika jamii,” alisema katika taarifa ya bajeti ya mwaka 2021/2022.

Mpango huo wa lazima wa kujiunga na NHIF kwa Wakenya wote umeboreshwa zaidi kinyume na ule uliopo sasa ambapo ni wafanyakazi katika sekta rasmi pekee wanaoshurutishwa kuwa wanachama.

You can share this post!

Mpango wa ‘Happy Hour’ warejeshwa kupunguza...

Jubilee yawaonya vikali madiwani wa ngome ya Ruto...