• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 8:55 PM
Jinsi ya kuandaa mlo mtamu wa biriani ya nyama ya mbuzi

Jinsi ya kuandaa mlo mtamu wa biriani ya nyama ya mbuzi

Na MARY WANGARI

WIKENDI ni wakati murwa sana wa kutangamana na kuwa na muda na familia na wapendwa.

Ni njia gani nyingine bora zaidi kama kufurahia wakati huo mkishiriki na kujiburudisha kwa mapochopocho ya chakula kitamu kilichoandaliwa kwa ustadi wa hali ya juu?

Hii leo tutajifahamisha jinsi ya kuandaa mlo mtamu wa biryani kwa nyama ya mbuzi.

Utahitaji viungo vifuatavyo

½ kilogramu ya mchele aina ya Basmati

¾ kilogramu ya nyama ya mbuzi

½ kilogramu mafuta ya kupikia

5 viazi mbatata vikubwa

1 karoti kubwa iliyoparwa

1 hoho iliyokatwa vipande vidogo vidogo

4 vitunguu maji vikubwa

4 nyanya kubwa

1 nyanya ya mkebe

I kijiko biryani masala

½ kijiko cha sukari

1kikombe cha mtindi au ukipenda maziwa yaliyogandishwa

½ kijiko cha chumvi unaweza ukongeza au kupunguza

1 ndimu moja kubwa au siki

1 kijiko cha iliki illiyotwangwa

1 kijiko cha tangawizi

1 kiijiko cha curry powder

Maji safi ya kupikia

Maandalizi

Safisha mchele na kisha uuroweke kwa maji robo saa.

Katakata nyama vipande vipande kisha uioshe na kuiweka katika karai safi.

Ongeza iliki, tangawizi, curry powder, chumvi na uchanganye viungo hivyo na nyama hadi vichanganyike vyema.

Menya vitunguum, vioshe, katakata vipande vyembamba vya mviringo na uviweke pembeni.

Menya viazi, vioshe na uviweke kando.

Saga nyama au uipare

Rosti la Biriani

Katika sufuria safi weka nyama na kuibandika kwenye moto wa wastan.

Iruhusu ikauke maji yake na kisha uongeze maji taratibu na usubiri itokote hadi kuwa laini.

Katika sufuria nyingine, mimina mafuta na kubandika kwenye moto kisha ongeza vitunguu na kuvikoroga koroga hadi vigeuke rangi kuwa ya dhahabu.

Toa vitunguu na kisha ukaange viazi mbatata kwa dakika chache, kisha kanga karoti, pilipili hoho na uongeze iliki.

Ongeza nyanya kwenye viazi na kuruhusu viive kwa dakika tatu.

Kisha mimina nyama na supu yake na kuacha mchanganyiko huo utokote kwa dakika kadhaa

Ongeza nyanya ya mkebe, siki na mtindi na kuviruhusu vitokote.

Ongeza viungo vilivyosalia kama vile pilau, biriani masala na sukari koroga na uace vichemke.

Ongeza vitunguu ulivyokaanga na kuweka kando hapo awali.

Ruhusu rosti lako litokote kwa dakika tano na kisha uepue.

Wali wa Biriani

Mimina maji kwenye sufuria safi na uongeze chumvi.

Yakishachemka, ongeza mchele na uache utokote kwenye moto wa wastan hadi uive.

Nyunyizia mafuta, funika na uruhusu ukauke maji.

Chukua rosti la biryani na weka kwenye wali wako kisha uchanganye vyema.

Biryani yako sasa ipo tayari kuliwa. Epua, pakua na ufurahie mlo wako.

You can share this post!

Brighton wapoteza penalti mbili nalo bao lao la utata dhidi...

Newcastle United na mbwa-mwitu Wolves nguvu sawa kwenye...