• Nairobi
  • Last Updated April 24th, 2024 10:08 PM
Fujo, hongo kwenye uchaguzi mdogo Nakuru

Fujo, hongo kwenye uchaguzi mdogo Nakuru

NA ERIC MATARA

WANAHABARI watatu wamepata majeraha kwenye ghasia ambazo zimeshuhudiwa Alhamisi asubuhi katika kituo cha kupigia kura cha Shule ya Msingi ya Milimani, Wadi ya London, Nakuru baada ya kundi la vijana kumvamia mbunge wa Lang’ata Nixon Korir.

Huku wakiharibu gari lake, vijana hao walidai kuwa mbunge huyo alikuwa akiwahonga wapigakura kwa maelfu ya pesa nje ya kituo hicho lili kubadilisha maamuzi yao debeni.

Polisi walilazimika kuwarushia vijana hao gesi ya kutoa machozi kutuliza hali katika eneo hilo ambapo uchaguzi mdogo bado unaendelea kwa sasa.

Msimamizi wa uchaguzi katika zoezi hilo Silas Rotich amewaamuru Bw Korir na wanasiasa wengine ambao ni wandani wa Naibu Rais William Ruto kuondoka eneo hilo.

Hata hivyo, wanasiasa hao, wanaojumuisha Seneta wa Nakuru Susan Kihika na mwenzake wa Elgeyo Marakwet Kipchumba Murkomen walikaidi agizo hilo na kuwalazimisha polisi kutumia nguvu kuwaondoa katika kituo hicho kwa vitoa machozi.

 

 

You can share this post!

Kituo cha OlympAfrica cha kukuza talanta za michezo kuanza...

Mwamba kurejea nyumbani Nairobi Railway Club ujenzi wa...