• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 8:55 PM
Barasa: Waliozua fujo Kabuchai wangali huru, tunaonewa kama wandani wa Ruto

Barasa: Waliozua fujo Kabuchai wangali huru, tunaonewa kama wandani wa Ruto

Na SAMMY WAWERU

MBUNGE wa Kimilili Bw Didmus Barasa amedai wandani wa Naibu wa Rais, Dkt William Ruto wanahangaishwa kwa sababu ya msimamo wao kisiasa.

Bw Barasa alisema Ijumaa waliozua rabsha mnamo Alhamisi wakati wa uchaguzi mdogo eneobunge la Kabuchai, Kaunti ya Bungoma hawakutiwa nguvuni.

Mbunge huyo alisema wanasiasa waliokamatwa kwa madai ya kuwa na silaha hatari kwenye magari yao, zinazosemakana zilipangiwa kutumika kuzua fujo wanaandamwa kwa sababu ya ajili ya kuegemea upande wa Dkt Ruto.

“Hatujawahi kupiga yeyote wala kutishia. Waliozua vurugu wangali huru hawakukamatwa,” akalalamik mbunge huyo.

Bw Barasa ni miongoni mwa wabunge wanne wa Tangatanga waliotiwa nguvuni.

Wanajumuisha Mabw Barasa (Kimilili), Nelson Koech Belgut), Wilson Logo (Chesumei) na seneta wa Nandi, Samson Cherargei.

Wanne hao wamefikishwa mahakamani Bungoma.

Uchaguzi mdogo wa Kabuchai ulizua ushindani mkali kati ya Joseph Majimbo Kalasinga wa chama cha Ford-Kenya, kinachoongozwa na seneta wa Bungoma Bw Moses Wetangula, na mgombea wa UDA, Evans Kakai.

Bw Kalasinga aliibuka kidedea kwa kuzoa kura 19, 274 akifuatwa na Kakai 6, 455. Chama cha UDA kinahusishwa na Dkt Ruto.

Kiti cha Kabuchai kilisalia wazi baada ya kifo cha aliyekuwa mbunge wa eneo hilo, Bw James Mukwe Lusweti, Desemba 2020.

You can share this post!

Tunakamatwa kwa sababu mtoto mwenye maono amezaliwa jijini...

Echesa akamatwe – Mutyambai