• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 8:55 PM
Raila asihi Wapwani wapitishe BBI

Raila asihi Wapwani wapitishe BBI

Na SIAGO CECE

KIONGOZI wa ODM, Bw Raila Odinga amekamilisha ziara yake Pwani kwa kuwarai wakazi waunge mkono mswada wa BBI, siku ya kura ya maamuzi itakapowadia.

Bw Odinga alisema kupitia mswada huo, masuala ya dhuluma za mashamba ambazo zimewaathiri wakaazi wa Pwani kwa muda mrefu yataangaziwa.

“Niko hapa kuwaambia mpige kura ya ‘ndiyo’ kwa sababu BBI ndiyo suluhu ya shida zenu zote. BBI ikifaulu itawaletea maendeleo mengi,” Bw Odinga Alisema ripoti ya TJRC itatekelezwa chini ya miezi sita baada ya BBI kupitishwa.Masuala mengine ambayo aliahidi wakazi ni kuboresha uchumi wa Bahari ambao ni muhimu kwa wapwani.

“BBI itaboresha uchumi wa bahari na kuwasiaidia wavuvi pia. Kuna njia nyingi za kisiasa za kufanya uvuvi ambazo zitawawezesha wavuvi kuvua kwenye maji ya kina kirefu. Wakati huu ni Wachina ambao wanavua kwenye maji yetu,” alieleza.

Bw Raila alisema mapendekezo ya kubadilisha katiba yataleta mabadiliko kisera na maisha ya wakazi.

Bw Raila pia aliwaandaa wenyeji kuwa tayari kwa kura ya maamuzi.Alisisitizia kwamba kupitia BBI tume itakayosimamia maswala ya vijana itabuniwa ishara kwamba changamoto za ajira kwa vijana itapata sulushisho na kuzikwa katika kaburi la sahau.

Pia, kutwakuwa na maeneo bunge ambayo yataongezwa iwapo BBI itapitishwa, kumaanisha kwamba pesa za maendeleo zitaongezeka na kumfikia mwananchi.

“Wale ambao hawaungi BBI hawataki pesa ziwafikie wananchi. Pesa zitakazotolewa kwa kila kaunti zitaiongezeko kutoka kwa asilimia 15 hadi 35 ambazo asilimia tano zitaenda katika kusaidia miradi ya vijana,” alisema Bw Raila.

You can share this post!

Wapwani wataka kummeza Yatani kuhusu Bandari

Leicester City wacharaza Brighton na kutua nafasi ya pili...