• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 8:55 PM
Kenya Cup: KCB yalemea Quins kwa jasho Kabras iking’aria Strathmore

Kenya Cup: KCB yalemea Quins kwa jasho Kabras iking’aria Strathmore

Na GEOFFREY ANENE

KCB ilitolewa kijasho kabla ya kuzima Kenya Harlequin nayo Blak Blad ikalazimisha sare dhidi ya Menengai Oilers katika mechi za raundi ya pili ya Ligi Kuu ya raga (Kenya Cup) iliyoshuhudia msisimko wa aina yake uwanjani RFUEA, Jumamosi.

Viongozi Kabras Sugar walitoka chini 0-3 na kunyamzisha Leos ya Chuo Kikuu cha Strathmore 35-9 uwanjani Impala Club katika mchuano mwingine.

Wanabenki wa KCB walionekana kupata mswaki walipoongoza Quins 22-6 wakati wa mapumziko jijini Nairobi. Hata hivyo, waliponea ufufuo wa wenyeji wao katika kipindi cha pili na kushinda pembemba 35-32.

Evin Asena, Xavier Kipng’etich, Joshua Chisanga na Mark Wandetto walifunga alama za Quins nao KCB wakavuna ushindi kupitia kwa alama za Martin Owila, Michael Wanjala, Darwin Mukidza na Cabrine Muhanga.

Mechi iliyofungua siku hapo Jumamosi kati ya Blak Blad ya Chuo Kikuu cha Kenyatta na Menengai Oilers ilikamilika nguvu sawa 12-12 uwanjani RFUEA.

  • Tags

You can share this post!

Wabunge 10 waitwa na NCIC kuhusu fujo

Waliozua fujo watatiwa adabu au ni vitisho baridi...