NA ASSUMPTA WAUSI
Kungwi ninayo barua, maisha kisulisuli
Nicheze yangu gitaa, ujumbe ufike mbali
Wifi ,halati bavyaa, mtambue minajili
Ubakaji ja makaa, uchoma tena vikali .
Kwa ami kaendelea, kulindwa kama kipuli
Nikaitwa malkia, kajisahau akili
Mtoto sasa nalia, ami kaniumia sili
Ubakaji ja makaa uchoma tena vikali.
Somo shangazi kaua, hauoni ufidhuli
Binamuzo nao pia, kauparamia mwili
Hila yote kanivamia, iko wapi serikali
Ubakaji ja makaa, uchoma tena vikali.
Nani wakunifidia, donda sawa na kivuli
Yaniuma kila saa, matendo haya katili
Asilimia ni mia, kilio changu ahali
Ubakaji ja makaa, uchoma tena vikali.
Yamekuwa mazoea, halati yu pilipili
Jumapili Ijumaa, nawaitaji wakili
Waondoe kitambaa, cheusi cha makali
Ubakaji ja makaa, uchoma tena vikali.