• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 12:30 PM
Rais Kenyatta atangaza siku 7 za kumwomboleza Magufuli, bendera nusu mlingoti

Rais Kenyatta atangaza siku 7 za kumwomboleza Magufuli, bendera nusu mlingoti

NA WANGU KANURI

RAIS Uhuru Kenyatta ametoa risala za rambirambi kwa mkewe Rais Magufuli, Janet Magufuli, watoto wao, jamaa na taifa la Tanzania kufuatia kifo cha kiongozi wa nchi hiyo. Rais Kenyatta aliwahakikishia wanaTanzania kuwa wapo kwenye fikra na maombi yetu.

“Afrika na dunia kwa ujumla imempoteza kiongozi wa kupigiwa mfano ambaye uongozi wake, bidii na maono yake yalifanya nchi ya Tanzania kupiga hatua za maendeleo. Pia Bw Magufuli alipigania umoja wa wanajumuiya ya Afrika Mashariki. Katika nchi za bara, marehemu Magufuli alipigania muungano wa Afrika. Kifo chake kimemnyakua rafiki na kiongozi mwenzangu,” akasema Rais Kenyatta.

Rais Kenyatta alisema anakumbuka wakati ambapo Rais Magufuli alizuru nchini Kenya kirasmi wakati wa uzinduzi barabara jijiniNairobi. Anakumbuka mazungumzo yao ambayo yalihusu maendeleo ya nchi zote mbili.

Alisimulia pia jinsi Bw Magufuli alisisitiza kwenda kumuona mamake Kenyatta, mama Ngina Kenyatta nyumbani kwao na akafunga safari ya kumtembelea almuradi amtoleee heshima.

Baada ya muda, marehemu Magufuli pia alimpeleka Rais Kenyatta kwao eneo la Chato, Geita, Tanzania na akamsalimu mamake Magufuli na kuongea naye kisha kulala kuko huko.

Safari hiyo iliwapa fursa ya kuzungumza mengi kuhusu uongozi wa nchi ya Kenya na Tanzania na pia uongozi wa jumuiya ya Afrika Mashariki kama wanachama.

Rais Kenyatta ambaye ni mwenyekiti wa Baraza la Jumuiya ya Afrika Mashariki ameagiza kuwa taifa la Kenya litatenga siku saba za kumuomboleza Bw Magufuli. Kwa wakati uo huo bendera ya Jumuiya ya Afrika Mashariki na ya nchi ya Kenya zitapeperushwa nusu ya mlingoti nchini Kenya na katika ubalozi wa Kenya kwa mataifa mengine.

“Bendera ya Kenya na ya Jumuiya ya Afrika Mashariki zitapeperushwa nusu mlingoti kutoka leo Machi 18, 2021 hadi machweo ya siku ambayo mwili wa rais Magufuli utakapozikwa. Bendera hizi zitapeperushwa katika majengo yote ya umma, nyanja zote za umma na katika ubalozi wa Kenya kwa mataifa mengine,” akasema rais Kenyatta.

Bw Magufuli alifariki Jumatano saa tano usiku huku ujumbe huu ukiwasilishwa naye makamu wa rais mheshimiwa Samia Suluhu. Magufuli alifariki baada ya kuugua ugonjwa wa moyo. Ameaga akiwa mwenye umri wa miaka 61.

Maisha yake

Mwendazake alizaliwa katika eneo la Chato, wilaya ya Geita kaskazini-magharibi mwa Tanzania mnamo Oktoba 1959 na alikuwa rais wa tano kuushika uongozi wa Tanzania tangu 2015 alipomshinda Edward Lowassa katika kinyang’anyiro kikuu nchini humo. Lakini hakulenga usiasa mwanzoni.

Magufuli alipata masomo yake yote nchini Tanzania na alikuwa mwalimu wa sayansi aliyefunza hisabati na kemia kisha baadaye akafanya kazi kama mkemia wa viwanda katika kampuni ya kumudu pamba la Nyanza, eneo la Mwanza kaskazini mwa Tanzania.

Aliteuliwa bungeni mnamo 1995, ambapo alihudumu kwenye baraza la mawaziri nchini Tanzania kama naibu Waziri wa Kazi kutoka mwaka wa 1995 hadi 2000, akahudumu kama Waziri wa Kazi tena kutoka mwaka wa 2000 hadi 2006, akahudumu kama Waziri wa Ardhi na Makazi ya Watu kutoka mwaka wa 2006 hadi 2008, akahudumu kama Waziri wa Mifugo na Uvuvi kutoka mwaka wa 2008 hadi 2010 na mwishowe akahudumu kama Waziri wa Kazi mara ya tatu mnamo mwaka wa 2010 hadi 2015.

Kama Waziri na kisha Rais, alipenda sana kupigiania utendaji bora kwa umma. Kampeni zake zililenga kukomesha ufisadi na kuziokoa fedha za umma pamoja na kulinda biashara za waTanzania.

Uongozi wa kwanza

Baada ya kuuchukua uongozi wa Tanzania mnamo 2015, aliweka mikakati ya kupunguza bei. Alipunguza usafiri wake wa bara na pia usafiri wake katika vikao vya wajumbe wa bara. Kwa mfano, alipunguza mkutano wa wajumbe wa Jumuiya ya madola, Uingereza hadi nne kutoka 50. Zaidi ya hayo, alielekeza pesa zilizonuiwa kuwa za vyakula vya jioni ama sherehe za umma kuwa za kuwasaidia wasiojiweza na wagonjwa.

Magufuli alipunguza mshahara wake kutoka milioni 1.5 kila mwezi hadi sh.400,000 na akawapunguza mawaziri hadi 15 ikilinganishwa na 30 wa Kikwete. Miezi michache baada ya kuteuliwa kwake mnamo mwaka wa 2015, hashtegi ya ‘Ni nini Maghufuli atafanya’ ilisambaa kwenye mitandao ya kijamii huku watu wan chi jirani wakipendezwa na utendakazi wake.

Chini ya uongozi wake Magufuli, IMF iliorodhesha Tanzania kama mojawapo wa nchi zilizokuza uchumi wao, kwa asilimia 6. Mwaka jana, benki kuu ya dunia ilikubali nchi hiyo iwe miongoni mwa kitengo cha nchi zenye uchumi wa chini na wa kati, hata ingawa mchakato huo utamalizika mwaka wa 2023.

Magufuli alijenga miundo mbinu kadha wa kadha kama ujenzi wa bandari ya Bagamoyo, bomba la mafuta kutoka Uganda, reli la SGR na ukuzi wa utaji wa usafiri wa hewani nchini Tanzania. Hata hivyo, cheo chake katika faharisi ya mtazamo wa ufisadi kimekwama. Tanzania ilijizolea nambari 94 kwa nchi 180 katika uratibu uliofanywa mwaka wa 2020. Ripoti kuhusiana na uhuru wa vyombo wa habari kutoka kwa waandishi wa habari wasio na mipaka (RSF) ilisema kuwa Tanzania ilirudi nyuma katika kuwapa vyombo vya habari uhuru wao.

RSF ilisema kuwa, “Hakuna nchi kati ya zile 180 zilizoorodheshwa na waandishi wasio na mipaka katika faharisi ya uhuru wa vyombo vya habari duniani ambayo imeshuka katika miaka iliyopita,” huku ikimlaumu Magufuli kwa kutostahimili kukosolewa yeye na sera alizounda.” RSF iliorodhesha nambari 124 kwa nambari 180 kwa Tanzania, huku nchi hiyo ikiwa imekuwa chini ya nchi sita hapo awali katika uratibu uliofanywa mwaka wa 2019.

Umaarufu 

Kesi iliyojulikana sana katika Jumuiya ya Afrika Mashariki ilimhusu Erick Kabendera aliyenyooshewa kidole cha lawama kwa kuandika kuhusu ufisadi wa vyombo vya habari vya bara. Kesi yake ilijikokota kwa miezi huku karatasi iliyonakiliwa makosa yake ikibadilishwa mara tatu. Mwishowe Kabendera alitozwa faini kwa utapeli wa pesa haramu, kutolipa ushuru na kuongoza uhalifu. Chini ya majadaliano hayo, Kabendera alilipa $120,000 kabla hajaachiliwa mnamo Februari mwaka jana.

Kundi za kuzitetea haki za binadamu zikiwemo Amnesty International na Human Rights Watch zilisema kuwa hukumu yake ilikuwa ya kisiasa. Licha ya umaaarufu wake wa kwanza nchini, upatanishi wake na wenyeji ulitiliwa shaka. Maghufuli aliwatembelea marais waliomtangulia mara chache sana huku serikali yake ikikwaruzana sana na nchi ya Kenya.

Mkwaruzano kati ya nchi hizi mbili ulisababisha kuzuiliwa kwa mifugo ilivyovuka mipaka, kuwachoma vifaranga walioletwa nchini Kenya, kupiga marufuku kuingia kwa magari ya ziara katika hifadhi na kutoelewana katika kudhibiti ugonjwa wa Covid-19. Katika mambo haya yote, suluhu ilipatikana baada ya muda.

Magufuli ametoa uamuzi unaopigana kwa mfano kubadilisha sheria za uchimabji wa madini ili kuruhusu nchi kutamatisha mikataba iwapo ulaghai unakisiwa na kuzikataza kampuni kushtaki Tanzania katika usuluhishi wa bara. Mojawapo ya kesi zinazoendelea ni kuhusu Acaia Gold ambayo Dar iliwalaumu kwa kuripoti viwango visivyofaa vya mauzo ya nje ya dhahabu.

Baada ya miaka ya maandamano, kampuni hiyo iliamua kufidia ushuru wa dola milioni 100 kwa serikali na ikahitajika kulipia nyongeza ya dola milioni 200 pamoja na kupokeza serikali hisa za asilimia 16. Mabishano mengine ni pamoja na kuagiza jeshi kununua korosho kutoka wakulima ili kuwaondoa walanguzi. Hali kadhalika, jeshi ilishindwa kufikia soko, huku ikishusha bei ya korosho. Pia Magufuli alilaumiwa kwa kuwalazimisha wanafunzi walioshika mimba kubaki nyumbani hata baada ya kuwapata watoto na kuziweka sera bishi za kuwasaka mashoga.

 

You can share this post!

Magavana Kenya wamwomboleza Rais Magufuli

Utawala wa Magufuli ulivyoua demokrasia Tanzania