• Nairobi
  • Last Updated April 24th, 2024 10:08 PM
China yaanza kutoa chanjo ya Covid-19 kwa wageni wa mataifa mbalimbali

China yaanza kutoa chanjo ya Covid-19 kwa wageni wa mataifa mbalimbali

Na MASHIRIKA

OFISI ya mambo ya kigeni jijini Beijing imesema Beijing imeanza kuwapa wageni wa mataifa mbalimbali chanjo ya Covid-19.

Kufuatia kanuni ya kushiriki kwa hiari, kutoa idhini binafsi na kubeba jukumu la hatari, wageni wa mataifa mbalimbali wenye umri wa miaka 18 na zaidi watapatiwa chanjo ya Covid-19.

Kwa mujibu wa taarifa, chanjo itakayotumika ni ya China na itahitaji dozi mbili.

Wageni wote wanaotaka kuchanjwa wanaweza kuangalia matangazo yatakayotolewa na waajiri wao, shule au ofisi za jamii ya makazi na kuweka miadi kupitia taasisi hizo.

Kufikia Machi 28, 2021 zaidi ya watu milioni 106 walikuwa wamepata chanjo katika maeneo mbalimbali kote nchini China.

Kwa sasa, maambukizi yote mapya yaliyoripotiwa nchini China ni kutokana na watu wanaoingia nchini humo. Ili kuzuia kuletwa kwa vyanzo vya nje vya maambukizi, China inaharakisha mchakato wa utoaji wa chanjo ili kuwezesha watu wengi kupata kinga.

CRI

 

You can share this post!

MUTUA AMTIA UHURU PRESHA

Watu 45 walifariki katika makanyagano wakitazama mwili wa...