• Nairobi
  • Last Updated April 25th, 2024 12:26 PM
IEBC yaidhinisha wawaniaji 6 wa ubunge Juja

IEBC yaidhinisha wawaniaji 6 wa ubunge Juja

Na LAWRENCE ONGARO

TUME ya uchaguzi ya IEBC iliwaidhinisha wagombezi sita wa ubunge katika kiti cha Juja. Zoezi hilo lililofanyika mnamo Jumatatu, lilimuidhinisha Bi Susan Njeri Waititu mjane wa marehemu Francis ‘ Wakapee’ Waititu atakaye peperusha mbendera na tikiti ya Jubilee.

Wengine walioidhinishwa huku wakijiandaa kuwania kiti hicho na tikiti ya ( Independent), ni Bw James Marungu Kariuki, Dkt Joseph Gichui, Bw Kariuki Ireri, Bw Chege Kariuki na Zulu Thiong’o.

Bi Waititu alikiri kuwa wao kama wawaniaji kiti hicho watapitia changa moto ya kujumuika na wapigaji kura kwa vikundi vikubwa.

Alisema wakazi wa Juja wangependa kuona mirandi yote yaliyoanzishwa yanakamilika ilivyopangwa.

” Iwapo nitapata hiyo nafasi ya kuwakilisha wakazi wa Juja bila shaka ajenda hizo zitaangaziwa zaidi,” alisema Bi Waititu.

Lakini hata hivyo alisema atatumia njia ya mtandao na mawasiliano na pia kutundika picha zake hadharani.

Afisa mkuu wa IEBC katika kaunti ndogo ya Juja, Bw Julius Mbithi, aliwahimiza wawaniaji wote wafuate mikakati yote iliyowekwa na wizara ya afya ili kukabiliana na homa ya covid-19.

Aliwajulisha wawaniaji hao kuwa sasa wana nafasi ya kuwania kiti cha Juja baada ya kuidhinishwa kirasmi na tume hiyo.

Uchaguzi mdogo wa Juja unatarajiwa kuendeshwa mwezi Mei 18, 2021, huku ukitarajiwa kuwa na upinzani mkali.

Kiti hicho kiliachwa wazi baada ya aliyekuwa mbunge wake Bw Francis ‘ Wakapee’ Waititu, kufariki baada ya kuugua saratani ya ubongo kwa zaidi ya miaka miwili.

Bw Kariuki ambaye pia anawania kiti hicho na tikiti ya (Independent), alisema watafanya juhudi kuona ya kwamba wanafuata maagizo yote yaliyowekwa na wizara ya afya.

” Tunaelewa vyema kuwa kuna changa moto lakini tutahakikisha tunawafikia wapigaji kura kwa njia ya mitadao na pia kutundika picha maeneo tofauti,” alifafanua .

Kiti cha ubunge cha Juja kimevutia wagombezi 10 ambapo wengine wanne waliosalia wataidhinishwa na tume ya uchaguzi mnamo Jumanne asubuhi.

Baadhi ya waliosalia ni Bw George Koimburi ( People Empowerment Party). Halafu kuna Anthony Kirori (Maendeleo Chap Chap), Eunice Wanjiru ( The National Democrat) na Kenneth Gachuma ( National Liberal Party).

You can share this post!

Harambee Stars yapiga Togo 2-1 bila Olunga

Maradhi Ya Kutatizwa Na Figo yaongezeka nchini