• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 6:25 PM
Ronaldo na Jota watambisha Ureno dhidi ya Luxembourg

Ronaldo na Jota watambisha Ureno dhidi ya Luxembourg

Na MASHIRIKA

WANASOKA Diogo Jota na Cristiano Ronaldo walifunga bao kila mmoja na kusaidia Ureno ambao ni mabingwa wa bara Ulaya kucharaza Luxembourg 3-1 mnamo Machi 30, 2021.

Luxembourg walishuka dimbani kwa ajili ya mechi hiyo wakijivunia kupepeta Jamhuri ya Ireland 1-0 katika mchuano wao wa awali wa Kundi A.

Waliwekwa uongozini dhidi ya Ureno kupitia kwa Gerson Rodrigues katika dakika ya 30 kabla ya Jota wa Liverpool kusawazisha mambo mwishoni mwa kipindi cha kwanza.

Ronaldo alifungia Ureno goli la pili mwanzoni mwa kipindi cha pili kabla ya Joao Palhinha kuzamisha kabisa chombo cha wenyeji wao katika dakika ya 80, muda mfupi kanla ya Maxime Chanot kuonyeshwa kadi nyekundu kwa kosa la kumchezea fowadi Renato Sanches visivyo.

Ureno wangalifunga mabao zaidi katika kipindi cha pili ila makombora ya Jota na Ronaldo yakadhibitiwa vilivyo na kipa Anthony Moris wa Luxembourg.

Ureno kwa sasa wanadhibiti kilele cha Kundi A kwa alama saba sawa na Serbia waliowalazimishia sare ya 2-2 mnamo Machi 27, 2021.

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Uholanzi yapepeta Gibraltar bila huruma katika gozi la...

Lewandowski kukaa nje kwa mwezi mmoja baada ya kupata...