• Nairobi
  • Last Updated April 24th, 2024 10:24 AM
Kocha Molefi Ntseki wa Bafana Bafana ya Afrika Kusini apigwa kalamu

Kocha Molefi Ntseki wa Bafana Bafana ya Afrika Kusini apigwa kalamu

Na MASHIRIKA

KOCHA Molefi Ntseki wa timu ya taifa ya Afrika Kusini almaarufu Bafana Bafana, amefutwa kazi baada ya kushindwa kuongoza kikosi chake kufuzu kwa fainali za Kombe la Afrika (AFCON) 2022 nchini Cameroon.

Kutimuliwa kwa Ntseki kulichochewa na matokeo duni yaliyosajiliwa na Bafana Bafana katika mechi mbili za mwisho za makundi ambapo waliambulia sare ya 1-1 dhidi ya Ghana nyumbani kisha wakazidiwa maarifa na Sudan kwa kichapo cha 2-0 ugenini.

Baada ya kukabwa koo na Ghana, Bafana Bafana walikuwa wakihitaji sare ya aina yoyote dhidi ya Sudan ili kujikatia tiketi ya kuelekea Cameroon mnamo Januari 2022.

Katika taarifa yake, Ntseki alikiri kwamba “kutofuzu kwa Afrika Kusini kwa fainali za AFCON kulikuwa kumesababishia raia wengi wa taifa hilo machungu na masumbuko ya kisaikolojia.”

TAFSIRI NA: CHRIS ADUNGO

  • Tags

You can share this post!

Lewandowski kukaa nje kwa mwezi mmoja baada ya kupata...

Cape Verde, Guinea-Bissau, Mauritania na Ethiopia pia...