• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 2:07 PM
Wanahabari wa spoti wa NMG watwaa tuzo

Wanahabari wa spoti wa NMG watwaa tuzo

Na MWANDISHI WETU

Wanahabari wa spoti wa kampuni ya Nation Media Group (NMG) walitawala hafla ya utoaji tuzo za Muungano wa Wanahabari wa Spoti Kimataifa (AIPS) 2020 kwa kutwaa mataji kwa wingi.

Tuzo hizo zilitolewa kwa waandishi wa spoti bora barani Afrika.Wanahabari hao wakiongozwa na mhariri wa spoti Elias Makori, walidhihirisha kwamba janga la corona halikuwa kizingiti kwao kujitolea na kujituma kazini.

Waandishi wa magazeti, Runinga na wa mitandaoni waliotambuliwa kwenye hafla hiyo ya Alhamisi jioni walijumuisha Elias Makori (Daily Nation) na Idah Waringa (NTV).

Ripota wa NTV Stephen Keter alitwaa taji la Mwanaripota bora Chipukizi Afrika huku mpigapicha wa Taifa Leo na Daily Nation Sila Kiplagat akiburura mataji mawili kwa kupiga picha za kusisimua.

Sila Kiplagat aliibuka bora zaidi barani katika kitengo cha mpigapicha chipukizi na kuchukua nafasi ya pili kwa kupiga picha murua za spoti.

Wengine ni? Jeff Kinyanjui, Samuel Gacharira na Cellestine Olilo wote wa Daily Nation. Idah Waringa alitwaa tuzo tatu.

Aliibuka wa kwanza barani Afrika kwa kuwa na stori bora zaidi kuhusu upelelezi. Waringa alipata matuzo mengine kwa kutoa video bora. Mhariri Elias Makori aliibuka wa pili barani wa kuandika stori iliyopendeza zaidi kuhusu kikosi cha Shujaa kilichoshirika mashindano jijini Vienna.

 

You can share this post!

Wakazi walia barabara mbovu zinawaletea hasara

Polisi ahepa kazi Mombasa kufukuzia penzi la mama...