• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 1:29 PM
‘Nimeandaa mapishi 25 kutoka nchi mbalimbali Afrika na Ulayani’

‘Nimeandaa mapishi 25 kutoka nchi mbalimbali Afrika na Ulayani’

Na MAGDALENE WANJA

Bi Ayumi Yamamoto alizaliwa na kulelewa katika mji wa Osaka nchini Japan ambapo alisoma na kuhitimu katika kozi ya Ukulima katika chuo kikuu.

Baadaye, alipata kazi ya kuwa mwalimu katika somo hilo hadimwaka 2011 alipoingia nchini Kenya.

Alisafiri hadi nchini Kenya kufanya kazi ya volunteer na shirika la Overseas Cooperative Volunteer ambalo ni shirika la serikali ya Japan.

Baada ya miaka miwili unusu,alianza biashara ya kuuza matunda yaliyokaushwa katika kampuni inayojulikana kama Kenya Fruits Solutions.

Alipokuwa akifanya kazi hizi, aligundua kwamba kulikuwana hitaji kubwa ya huduma za kuwapelekea wateja chakula(delivery) katika nyumba zao mjini Nairobi.

Aliwaza jinsi angeweza kuleta suluhisho katika sekta hii na akaamua kutengeneza mealkits.

“Baada ya kufanya kazi katika sekta mbalimbali za lishe, nilitamani sana kufanya biashara ya kuuza ama kuandaa chakula” alisema Yamamoto.

“Nilishangazwa piana insihitaji la chakula liliendelea kukua kila siku mjini Nairobina nikaiona kama nafasi nzuri ya biashara,” aliongeza Yamamoto.

Baadhi ya vyakula anavyoandaa Bi Ayumi Yamamoto. Picha- MAGDALENE WANJA

Baada ya kufanya matayarisho yote mnamo mwaka 2019, aliweza kuanzisha kampuni yake ambayo aliiita Love and Meals.

Wazo lake la kutengeneza Meal Kits pia lilichangiwa na ujuzi alioupata kutoka kwa watu aliotangamana naokutoka sehemu mbalimbali ulimwenguni.

Ndani ya meal kit, Bi Yamamoto humuandalia mteja wake vinavyohitajika kuandaa aina fulani ya chakula kisha anakuandalia maandishi ya muongozo wa jinsi ya kukitayarisha chakula hicho.

Kwa meal kit moja,kampuni yake hulipisha kuanzia Sh1,050 ambayo pia huhuandamana na iloe ya usafirishaji.

Huduma hii hupatikana mtandaoni ambapo mteja hujichagulia anachohitaji na kasha kupeana maagizo kupitia program hio ya simu.

“Lengo letu ni kuwafanya wateja wetu kuridhika na huduma zetu huku tukirahisisha kazi ya upishi haswa kwa watu ambao hawana muda wakutosha wa kujiandalia mlo wanaotaka kutokana na ukosefu wa muda au kutojua jinsi ya kuandaa,” aliongeza.

Kufikia sasa, Yamamoto ameweza kuandaa mapishi 25 kutoka nchi mbalimbali barani Afrika na Ulayani.

Ndoto yake ni yake ni kuendeleza huduma zake katika miji mingine mikuu nchini na mataifa mengine.

You can share this post!

ODM yasema Raila amepona corona

Kiungo wa Bandari asifiwa na Adebayor