• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 11:38 AM
Hazina ya Kitaifa yalaumiwa kwa uzorotaji wa huduma vituo vya afya Kakamega

Hazina ya Kitaifa yalaumiwa kwa uzorotaji wa huduma vituo vya afya Kakamega

SHABAN MAKOKHA na CHARLES WASONGA

HATUA ya Hazina ya Kitaifa kuchelewesha utoaji wa fedha kwa kaunti imechangia kuzorota kwa hali ya utoaji huduma katika vituo vya kiafya katika Kaunti ya Kakamega.

Waziri wa Afya katika kaunti hiyo Dkt Collins Matemba Alhamisi alisema uhaba wa fedha umechangia kaunti hiyo kulemewa kuendesha shughuli zake.

“Tumepokea fedha mara tano pekee tangu Mwaka wa Kifedha wa 2020/2021 ulipoanza. Hali hii imeathiri pakubwa shughuli zetu na hivyo kukwama kwa huduma katika vituo mbalimbali,” akasema Dkt Matemba.

Waziri huyo alikuwa akimjibu Mbunge wa Matungu Peter Nabulindo ambaye amependekeza kufungwa hospitali ya kaunti ndogo ya Matungu kutokana na hali mbaya katika hospitali hiyo.

Mbunge huyo alisema baadhi ya wagonjwa waliolazwa katika wadi za hospitali hiyo hawana chakula.

Wananchi katika eneo hilo wamelalamikia hali mbaya ya hospitali na kuitaka serikali ya Kaunti ya Kakamega kutoa suluhu kwa changamoto kadha zinazoikabili.

  • Tags

You can share this post!

Kenya yaomba mkopo mwingine wa Sh86 bilioni kutoka Benki ya...

Supamaketi zina kibarua kudhibiti msongamano wa watu...