• Nairobi
  • Last Updated April 24th, 2024 5:39 PM
Huduma za ukaguzi magari kutekelezwa kila Ijumaa mjini Murang’a

Huduma za ukaguzi magari kutekelezwa kila Ijumaa mjini Murang’a

Na MWANGI MUIRURI

KAMISHNA wa Kaunti ya Murang’a Bw Mohamned Barre ametangaza Ijumaa kuwa huduma za ukaguzi wa magari zitaanza kutolewa na Mamlaka ya Usalama Barabarani Nchini (NTSA) kila Ijumaa mjini Murang’a.

Bw Barre ametangaza kuwa hatua hiyo imeafikiwa kufuatia ugumu wa wamiliki wa magari katika kaunti hiyo kuzimwa kupata huduma hizo katika miji ya Nairobi na Thika kufuatia ‘lockdown’ iliyowekwa kupambana na janga la Covid-19 Rais Uhuru Kenyatta alipotangaza Machi 26.

Kamishna amesema marufuku hayo yamesababishia wengi kutatizika kwa kuwa ni kinyume na sheria za trafiki kuendesha gari ambalo halina cheti cha ukaguzi.

Bw Barre ametangaza kuwa maafisa wa NTSA sasa watakuwa wakikita kambi kila Ijumaa katika karakana ya Wizara ya Uchukuzi iliyoko katika barabara ya Kutoka Murang’a hadi Sagana.

“Serikali imetambua kuwa kuna shida kubwa kwa wamiliki wa magari wakisaka huduma hizi za ukaguzi. Mikakati hii ni ya kutatua shida hiyo na tutakuwa tukitekeleza wajibu huo kila Ijumaa,” akasema.

Aidha Bw Barre ametangaza kuwa leseni za kisasa zinazotolewa kidijitali zitaendea kupeanwa kwa waliojisali kila ijumaa ya wiki katika kituo cha Huduma Kilichoko Mjini Murang’a.

  • Tags

You can share this post!

Visa vya wizi wa ng’ombe vyazidi Gatundu Kaskazini

Ombi la kuchangishia shujaa Ayimba ambaye ni mgonjwa Sh2...