• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 6:50 PM
Ombi la kuchangishia shujaa Ayimba ambaye ni mgonjwa Sh2 milioni

Ombi la kuchangishia shujaa Ayimba ambaye ni mgonjwa Sh2 milioni

Na GEOFFREY ANENE

KOCHA na mchezaji wa zamani wa timu ya taifa ya raga ya wachezaji saba kila upande ya Kenya, Benjamin Ayimba anahitaji msaada wa Sh2 milioni kufanikisha matibabu yake.

Ayimba maarufu kama Benja amekuwa akizuru hospitali mara kwa mara tangu mwaka 2020 baada ya kupatikana na ugonjwa wa malaria ya ubongo.

“Hali yake imezorota kwa haraka na anahitaji msaada wetu wakati huu kuliko wakati mwingine katika maisha yake,” Shirikisho la Raga Kenya (KRU) limesema Aprili 9, likimtaja kama shujaa wa kweli aliye hai na wa kitaifa.

“Tunaomba wahisani kuchangia katika kumsaidia apate matibabu mazuri ya kumrejesha katika hali nzuri ya kiafya. Mchango wa kiasi chochote utasaidia,” KRU ilisema na kutangaza nambari ya Paybill kuwa 8021673 akaunti Benjamin Otieno Medical.

Kabla ya kuwa kocha mkuu wa Shujaa zaidi ya miaka 10 iliyopita, Ayimba alikuwa nahodha wa timu hiyo kati ya mwaka 2000 na 2005 ikishiriki pia Kombe la Dunia mwaka 2001 nchini Argentina na 2005 Hong Kong.

Yeye ndiye kocha wa Shujaa ambaye amewahi kuongoza timu hiyo kutwaa taji kwenye mashindano ya kifahari ya Raga za Dunia. Alikuwa usukani akisaidiwa na Paul Murunga wakati Shujaa iliduwaza miamba Fiji 30-7 katika fainali ya Singapore Sevens mwaka 2016.

You can share this post!

Huduma za ukaguzi magari kutekelezwa kila Ijumaa mjini...

Gor na Leopards mashakani