• Nairobi
  • Last Updated April 18th, 2024 12:45 AM
Sakaja amshukuru Rais Kenyatta kwa kutoa Sh1 milioni kumfaa Ayimba

Sakaja amshukuru Rais Kenyatta kwa kutoa Sh1 milioni kumfaa Ayimba

Na GEOFFREY ANENE

RAIS Uhuru Kenyatta amekuwa mstari wa mbele kuitikia wito wa kuchangishia kocha wa zamani wa Timu ya Shujaa, Benjamin Ayimba ambaye ni mgonjwa.

Mchango wa Rais Kenyatta wa Sh1 milioni ulitangazwa na Seneta wa Kaunti ya Nairobi Johnson Arthur Sakaja kupitia mtandao wake wa Twitter mnamo Aprili 10.

Mnamo Aprili 9, familia ya Ayimba pamoja na Shirikisho la Raga Kenya (KRU) lilitangaza kuwa nahodha huyo wa zamani wa timu za taifa za raga ya wachezaji saba kila upande na ile ya wachezaji 15 kila upande anahitaji Sh2 milioni kufanikisha matibabu yake.

Iliitisha msaada kutoka kwa wahisani kupitia nambari ya Paybill ya 8021673 jina la akaunti likiwa ni Benjamin Otieno Medical.

“Benja amekuwa akifika hospitali mara kwa mara kupokea matibabu tangu mwisho wa mwaka 2020 baada ya kuchunguzwa kiafya na kupatikana anaugua malaria ya ubongo. Afya yake imezorota kwa haraka na anahitaji usaidizi wetu sana. Tunaomba wahisani kusaidia kutoa mchango wowote wa kifedha kufanikisha matibabu bora kuhakikisha anarejelea hali nzuri. Bili yake ya hospitali kwa sasa ni zaidi ya Sh2 milioni. Maombi yako na mchango wako utamfaa sana,” KRU ilisema.

You can share this post!

JAMVI: Kilio IEBC ikiendelea na chaguzi ndogo bila ya...

TAHARIRI: Kudungwa chanjo hakutozuia corona