• Nairobi
  • Last Updated April 18th, 2024 9:15 PM
Wanafunzi wa nchi za nje wapenda vyuo vikuu vya nchini Kenya

Wanafunzi wa nchi za nje wapenda vyuo vikuu vya nchini Kenya

Na LAWRENCE ONGARO

CHUO Kikuu cha Mount Kenya (MKU) kimeorodheshwa cha tano kupendwa na wanafunzi kutoka bara la Afrika na nje ya bara hili.

Utafiti huo uliofanywa majuzi na shirika la utafiti la CPS Research International unatoa maelezo kuwa MKU inapendwa pia na wanafunzi hao kutokana na mpangilio mwafaka uliopo huko.

Shirika hilo liko nchini Kenya na limekuwa likifanya utafiti wa kutathmini jinsi vyuo tofauti vinavyoendesha mipango ya elimu.

Kwa vyuo vya kibinafsi, MKU imeorodheshwa ya tatu nchini kwa kupata wanafunzi kutoka nje ya nchi, halafu pia ilipata nafasi ya nne kwa ubora wa mpangilio wake kielimu ikizoa alama za asilimia 57.05.

MKU imekuwa mstari wa mbele kwa maswala ya kufanya utafiti na ubunifu katika maswala ya elimu.

Baadhi ya maswala muhimu yanayowapa ari wanafunzi kutoka nchi za nje kufika MKU, ni ubora wa elimu, sifa zake, ushirikiano uliopo na jinsi wanavyowakuza wanafunzi chuoni.

Jambo jingine linalovutia wanafunzi kufika kwa baadhi ya vyuo vya nchini Kenya ni elimu ya hali ya juu, kupata malazi kwa njia ifaayo, muda mwafaka wa masomo uliowekwa na masomo kukamilika wakati bora zaidi bila kuchelewa.

Pia wanafunzi wengi kufika nchini kutafuta elimu ya juu kwa sababu ya sheria za kusafiri zilizopo, hali ya usalama, utamaduni uliopo, na mazingira mema ya kuishi.

Kulingana na utafiti huo Chuo Kikuu cha Nairobi (UoN) kina wanafunzi wengi kutoka nchi za nje ambapo idadi yao inafika 1,300. Nafasi ya pili ni Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Amerika – Kenya (USIU-Kenya) ambacho kina wanafunzi wapatao 1,100. Nafasi ya tatu inakamatwa na Chuo Kikuu cha Strathmore ambacho kinahifadhi wanafunzi 660.

  • Tags

You can share this post!

Kiptanui na Tanui waibuka washindi wa Xiamen Siena Marathon

Raila Odinga, Rais Kenyatta watoa mamilioni kusaidia...