• Nairobi
  • Last Updated March 28th, 2024 9:35 PM
Raila Odinga, Rais Kenyatta watoa mamilioni kusaidia matibabu ya Benjamin Ayimba

Raila Odinga, Rais Kenyatta watoa mamilioni kusaidia matibabu ya Benjamin Ayimba

Na GEOFFREY ANENE

KIONGOZI wa ODM, Raila Odinga hajaachwa nyuma katika kuchangishia kocha wa zamani wa timu ya Kenya Shujaa Benjamin Otieno Ayimba ambaye ni mgonjwa.

Siku moja baada ya Rais Uhuru Kenyatta kuwa wa kwanza kujitokeza na mchango wa Sh1 milioni, Bwana Odinga ametoa kiasi sawa na hicho.

Michango hiyo miwili ilitangazwa na Seneta wa Kaunti ya Nairobi Johnson Arthur Sakaja kupitia mtandao wake wa Twitter mnamo Aprili 10 na Aprili 11.

Mnamo Aprili 9, familia ya Ayimba pamoja na Shirikisho la Raga Kenya (KRU) lilitangaza kuwa nahodha huyo wa zamani wa timu za taifa za raga ya wachezaji saba kila upande na ile ya wachezaji 15 kila upande anahitaji Sh2 milioni kufanikisha matibabu yake.

Iliitisha msaada kutoka kwa wahisani kupitia nambari ya Paybill ya 8021673 jina la akaunti likiwa ni Benjamin Otieno Medical.

“Benja amekuwa akifika hospitali mara kwa mara kupokea matibabu tangu mwisho wa mwaka 2020 baada ya kuchunguzwa kiafya na kupatikana anaugua malaria ya ubongo. Afya yake imezorota kwa haraka na anahitaji usaidizi wetu sana. Tunaomba wahisani kusaidia kutoa mchango wowote wa kifedha kufanikisha matibabu bora kuhakikisha anarejelea hali nzuri. Bili yake ya hospitali kwa sasa ni zaidi ya Sh2 milioni. Maombi yako na mchango wako utamfaa sana,” KRU ilisema.

  • Tags

You can share this post!

Wanafunzi wa nchi za nje wapenda vyuo vikuu vya nchini Kenya

Fahamu muda sahihi unaopaswa kula matunda