• Nairobi
  • Last Updated April 19th, 2024 8:55 PM
China kuchanganya chanjo mbalimbali kukabili corona

China kuchanganya chanjo mbalimbali kukabili corona

NA AP

CHINA inapanga kuchanganya chanjo zake za kukabili virusi vya corona na chanjo kutoka nchi zingine ili kuimarisha ubora wake.

Mamlaka ya Kudhibiti Magonjwa nchini humo (CCDC), ilikiri kwamba ubora wa chanjo zake “uko chini” hivyo pana haja ya kuzichanganya na chanjo zingine ili kuziboresha zaidi.

“Chanjo za China hazina uwezo mkubwa kumzuia mtu kuambukizwa corona,” akasema Gao Fu, ambaye ndiye mkurugenzi mkuu wa mamlaka hiyo.

China imesambaza mamilioni ya dozi za chanjo zake katika nchi mbalimbali duniani, kwenye juhudi zinazoonekana kama mikakati ya kukabili chanjo kutoka nchi za Magharibi.

“Ni rasmi kwamba tumeanza kutathmini ikiwa tutakuwa tukitumia chanjo tofauti kuwachanja raia,” akasema Gao, alipohutubia wanahabari katika mji wa Chengdu, mkoa wa Sichuan.

Utathmini uliofanyiwa chanjo aina ya Sinovac kutoka China nchini Brazil, ulionyesha ina uwezo wa kiwango cha asilimia 50.4 kuwalinda watu dhidi ya corona. Hii ni ikilinganishwa na chanjo ya kampuni ya Pfizer kutoka Amerika, ambayo ina uwezo wa asilimia 97.

You can share this post!

Waziri Mkuu asema hatahudhuria mazishi ya mume wa Malkia...

Wazee wa Kaya watishia kulaani waliosingizia Naibu Gavana