• Nairobi
  • Last Updated April 23rd, 2024 6:55 PM
MAPISHI: Kuku kienyeji

MAPISHI: Kuku kienyeji

Na MARGARET MAINA

[email protected]

Muda wa kuandaa: Dakika 1

Muda wa mapishi: Saa 1

Walaji: 4

Vinavyohitajika

· kuku wa kienyeji 1

· vitunguu maji 3

· vitunguu saumu punje 2 zilizobondwa

· unga wa binzari

· pilipili manga

· mafuta ya kupikia

· giligilani

· tangawizi

· nyanya tatu

· juisi ya limau

Maelekezo

Katakata na uchemshe kuku wako pamoja na tangawizi, kitunguu saumu, unga wa binzari, pilipili manga, chumvi na ndimu ili kuweka ladha nzuri.

Acha vipande vya kuku viive.

Nyama ya kuku ikishaiva itoe katika supu na uiweke pembeni.

Katika sufuria tofauti, tia mafuta ya kupikia na yakishachemka, kaanga kuku wako hadi awe rangi ya kahawia. Kisha toa minofu ya kuku katika mafuta ili utumie mafuta hayo kwa kuweka vitunguu na ukaange kwa dakika tano.

Sasa weka unga wa binzari, unga wa giligilani, na mbegu za pilipili manga.

Changanya vizuri hadi upate mchanganyiko mzuri mkavu halafu miminia humo ile supu uliyoiacha hapo awali.

Weka pembeni ipoe kisha kaanga nyanya zako katika sufuria tofauti vile vile na upike hadi maji yaishe na ibakie kama mafuta yakielea kwa juu.

Mimina sosi yako katika kuku na punguza moto acha vichemke ili viungo vichanganyike na kuleta ladha nzuri. Utakapoona mchuzi umeisha, unaweza epua na kuweka pembeni.

Hapo nyama ya kuku itakuwa tayari kuliwa na chochote utakachopenda.

You can share this post!

Equator Rally kushuhudia kivumbi kikali magari saba ya...

Vyoo vya soko la Witeithie vyabomolewa