• Nairobi
  • Last Updated April 16th, 2024 4:37 PM
Mbwa wa Biden kupewa mafunzo mapya

Mbwa wa Biden kupewa mafunzo mapya

Na AFP

MBWA wa Rais wa Amerika Joe Biden, anayefahamika kama Major, atapelekwa kupokea mafunzo zaidi kuhusu jinsi ya kuwa na tabia ya mbwa wa rais.

Msemaji wa Mke wa Rais Jill Biden, Michael LaRosa, alisema Major atapokea “mafunzo ya ziada ya kumsaidia kuzoea maisha katika White House”.

“Mafunzo hayo ya siri yatafanyika katika eneo la Washington, DC na yanatarajiwa kuchukua muda wa wiki chache,” alisema LaRosa.

Mabadiliko hayo ya kuhamia ghafla Ikulu ya White House yalimchanganya mbwa huyo aina ya German Shepherd, aliyekuwa mbwa wa shughuli ya uokoaji.

Mnamo Machi, alirejeshwa katika makao ya familia ya Biden, mjini Delaware, baada ya kuuma watu wasiopungua wawili katika Ikulu.

Rais Biden alieleza vyombo vya habari Machi kwamba rafikiye alikuwa tu akilinda vikali jengo la White House lenye msongamano wa watu.

 

You can share this post!

Mfungo wa Ramadhan bila sherehe kwa mwaka wa pili

GSU yataja kikosi, itasafiri Alhamisi kwa mashindano ya...