• Nairobi
  • Last Updated March 29th, 2024 11:38 AM
UDAKU: Melanie awachoka visura kudonadona penzi lake na Martial

UDAKU: Melanie awachoka visura kudonadona penzi lake na Martial

Na CHRIS ADUNGO

KIPUSA Melanie Da Cruz ambaye ni mkewe mwanasoka Anthony Martial wa Manchester United, amechoshwa na vichuna wanaomvizia mumewe kimapenzi.

Melanie, 29, ni mwanamitindo na mwanahabari maarufu nchini Ufaransa.

Amekuwa akila bata na Martial, 25, tangu 2016 baada ya mshambuliaji huyo kutemana rasmi na mrembo Samantha Jacquelinet aliyemzalia mtoto wa kwanza, Peyton.

Kwa mujibu wa Melanie, kuwa mke wa mwanasoka maarufu kunahitaji moyo wa chuma. Aidha, akiri maisha si mepesi kama wengi wanavyodhania.

Akihojiwa na gazeti la French Football News wiki jana, Melanie alitishia kufunganya virago na kujiendea zake iwapo Martial hatakoma kuwasiliana mara kwa mara na warembo wanaomtumia picha za uchi mitandaoni ili kumuingiza boksi amege tunda.

“Kuwa mke wa Martial si tu kujivunia mabegi, mavazi, magari ya kifahari au hela nyingi. Sikuwahi kuwazia kuwa mke wa mwanasoka lakini nilijipata nikiwa na Martial.

“Tatizo ni kwamba anawaniwa sana na vichuna wa kila sampuli, na hilo linauma kwa yeyote mwenye moyo mwepesi,” akasema Melanie.

Aliongeza: “Nilishapata namba ya kudumu moyoni mwa Martial, ambaye kwa sasa anapania kunifanya wake wa halali. Yasikitisha kwamba wapo wasiolala kwa ajili ya Martial; itakuwa vyema wakimkoma.”

Mwishoni mwa mwaka jana, Melanie Da Cruz alitishia kumtema Martial kutokana na ukali wa jicho la nje baada ya straika huyo wa United kuanza kuchovya mwanamitindo wa Ufaransa, Malika Semichi.

Wakati huo, Melanie alidai kuwa Martial alivutiwa na mademu wa umri mdogo na akawa akimpangia Malika, 22, ziara za mara kwa mara kuponda raha jijini Paris, Ufaransa, tangu ajifungue mtoto Swan mnamo Julai 2018.

“Hatua ya Martial kuanza kutoka kimapenzi na vidosho wa rika lake iliniyima raha. Nilijutia kufahamiana naye kwa kuwa nilihisi kiini cha tabia yake hiyo ni umri wangu mkubwa, sababu namzidi kwa takriban miaka mitano,” alifichua Melanie.

Akihojiwa na gazeti la The Sun mwanzoni mwa juma lililopita, Samantha kwa upande wake alikiri kwamba kusambaratika kwa ndoa yake na Martial kulichangiwa na mwanamuziki Emily Wademan, aliyeanza kumwanikia mwanasoka huyo buyu lake la asali mara kwa mara tangu mwanzoni mwa 2016.

Baada ya jaribio la Samantha kurudiana na Martial kufeli, kidosho huyo alianza kumpaka tope Melanie akidai kwamba alikuwa hawara aliyeiba penzi la mumewe kwa nia ya kuzifakamia hela za staa huyo.

Hadi kufikia mwisho wa mwaka jana, Samantha alikuwa akiteswa na uhalisia wa kuyakosa mapenzi motomoto ya Martial ambaye alionekana akiponda raha na Melanie nchini Mauritius kabla ya kutua baadaye Santorini kisha Dubai.

“Nilishapata namba ya kudumu moyoni mwa Martial ambaye kwa sasa anapania kunifanya wake wa halali. Yasikitisha kwamba wapo wasiolala kwa ajili ya Martial na itakuwa vyema wakimkoma,” Melanie alinukuliwa na gazeti la French Football News.

You can share this post!

UDAKU: Foden kijogoo! Anawika uwanjani na chumbani pia

MBWEMBWE: Bruno Fernandes si magoli tu pia kuunda pesa...