• Nairobi
  • Last Updated April 20th, 2024 3:03 PM
Mfumo mpya wa wasaka-kazi kuwafaa vijana

Mfumo mpya wa wasaka-kazi kuwafaa vijana

Na MARY WANGARI

VIJANA nchini Kenya huenda wakanufaika pakubwa kutokana na nafasi za ajira katika sekta za umma na za kibinafsi kufuatia kubuniwa kwa mfumo maalum unaohifadhi data za wanaosaka ajira.

Mfumo huo mpya wa kielektroniki unalenga vijana wanaojiunga na kufuzu kutoka Shirika la Huduma ya Vijana kwa Taifa (NYS).

Akizungumza Jumamosi mjini Gilgil, Kaunti ya Nakuru alipozindua teknolojia hiyo, Rais Uhuru Kenyatta alisema mfumo huo mpya utawezesha kufuatilia, kuhifadhi rekodi na kurahisisha mchakato wa waajiri kuteua waajiriwa miongoni mwa mahafala wa NYS.

“Serikali imejitolea kubuni nyadhifa za kazi kwa vijana katika sekta za umma na za kibinafsi. Kuhusiana na hili, NYS imebuni mfumo unaohifadhi data ya mahafala wake kwa njia inayowezesha waajiriwa kuipata kirahisi,” alisema Rais Kenyatta.

Rais aliyekuwa akizungumza katika hafla ya kufuzu kwa mahafala 7,479 wa NYS, alifafanua kuwa teknolojia hiyo itawezesha waajiri kuteua wafanyakazi wenye ujuzi unaohitajika katika eneo fulani.

You can share this post!

Mfumo wa haki wa kitamaduni waokoa kaka walioua jamaa

Gavana bado katika hatari