• Nairobi
  • Last Updated April 23rd, 2024 10:10 AM
Watatu wafariki lori na matatu zikigongana mjini

Watatu wafariki lori na matatu zikigongana mjini

Na WACHIRA MWANGI

WATU watatu walifariki jana kwenye ajali iliyotokea katika Barabara ya Makupa, Kaunti ya Mombasa.

Kamanda wa Trafiki katika ukanda wa Pwani, Bw Peter Maina, alithibitisha kutokea kwa ajali hiyo, iliyohusisha matatu na lori.

Kulingana na walioshuhudia, matatu hiyo ilipoteza mwelekeo na kugongana na lori hilo lililokuwa likielekea Mombasa.

Matatu hiyo ambayo inamilikiwa na Kampuni ya Matco Sacco iliondoka jijini Mombasa asubuhi ikielekea Kitui wakati ajali hiyo ilipofanyika.

Dereva wa lori hilo, Bw Daniel Omondi, alisema alibahatika sana kunusurika ajali hiyo pamoja na kondakta wake.

“Matatu hiyo ilikuwa ikisafiria upande wangu. Nusura nitumbukie baharini kwani nilikuwa nikijaribu kuepuka kugongana nayo. Hata hivyo, iliingia upande wangu ndipo ajali ikatokea,” akasema Bw Omondi aliyeongeza kuwa alikuwa amesafiri usiku kucha kutoka Nairobi.

Miili ya waliofariki ilipelekwa katika mochari ya Hospitali ya Rufaa ya Coast General.

You can share this post!

Tangatanga wapinga vikali mswada wa BBI

RAMADHAN: Kufunga Ramadhani si mateso bali zawadi kwa...